10 Basi Loti akainua macho yake na kuona Wilaya yote ya Yordani,+ kwamba yote ilikuwa eneo lililokuwa na maji mengi kabla Yehova hajaharibu Sodoma na Gomora, kama bustani ya Yehova,+ kama nchi ya Misri mpaka Soari.+
18 Nitafungua mito juu ya vilima vitupu, na mabubujiko katikati ya nchi tambarare za bondeni.+ Nitaifanya nyika kuwa dimbwi la maji lenye matete mengi, na nchi isiyo na maji kuwa chemchemi za maji.+
8 Mierezi mingine haikulingana nao katika bustani ya Mungu.+ Nayo miberoshi, haikufanana nao kwa habari ya matawi yake. Na miaramoni yenyewe haikuwa kama huo katika matawi yake. Hakuna mti mwingine wowote katika bustani ya Mungu uliofanana nao katika uzuri wake.+