6 Nami nitaweka amani katika nchi,+ nanyi mtalala, pasipo yeyote wa kuwatetemesha;+ nami nitamkomesha katika nchi+ mnyama-mwitu mwenye madhara, nao upanga hautapita katika nchi yenu.+
6 Na mbwa-mwitu kwa kweli atakaa pamoja na mwana-kondoo+ kwa muda fulani, na chui atalala pamoja na mwana-mbuzi, na ndama na mwana-simba mwenye manyoya shingoni+ na mnyama aliyelishwa vizuri wote pamoja;+ na mvulana mdogo atakuwa kiongozi juu yao.
9 Hakuna simba atakayekuwa hapo, na wanyama-mwitu wenye kunyafua hawatakuja juu yake.+ Hakuna yeyote atakayepatikana hapo;+ na waliokombolewa watatembea hapo.+
25 “Mbwa-mwitu+ na mwana-kondoo watalisha kama kitu kimoja,+ na simba atakula majani kama ng’ombe;+ na kuhusu nyoka, chakula chake kitakuwa mavumbi.+ Hawatadhuru+ wala kufanya uharibifu wowote katika mlima wangu wote mtakatifu,”+ Yehova amesema.
18 Na kwa ajili yao hakika nitafanya agano siku hiyo na mnyama wa mwituni+ na kiumbe kinachoruka cha mbinguni na kitu kinachotambaa cha nchi, nami nitavunja kutoka katika nchi upinde na upanga na vita,+ nami nitawafanya walale salama salimini.+