12 Isitoshe, Absalomu alipotoa dhabihu, aliwatuma watu wamwite Ahithofeli+ Mgiloni, mshauri wa Daudi,+ kutoka jiji la Gilo.+ Njama iliendelea kupamba moto, na idadi ya watu waliomuunga mkono Absalomu ikaendelea kuongezeka.+
14 Ndipo Absalomu na wanaume wote wa Israeli wakasema: “Ushauri wa Hushai Mwarki ni bora+ kuliko ushauri wa Ahithofeli!” Kwa maana Yehova alikuwa ameazimia* kuvuruga ushauri mzuri wa Ahithofeli,+ ili Yehova amletee msiba Absalomu.+
23 Ahithofeli alipoona kwamba ushauri wake haukufuatwa, aliweka matandiko juu ya punda wake na kwenda nyumbani kwake katika mji wao.+ Baada ya kuwapa maagizo watu wa nyumbani mwake,+ akajitia kitanzi.*+ Basi akafa na kuzikwa katika makaburi ya mababu zake.