-
2 Mambo ya Nyakati 16:13, 14Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
13 Kisha Asa akafa na kuzikwa pamoja na mababu zake;+ alikufa katika mwaka wa 41 wa utawala wake. 14 Kwa hiyo walimzika katika kaburi lake la kifahari alilokuwa amejichimbia katika Jiji la Daudi;+ walimlaza kwenye machela ya kubebea maiti iliyojazwa mafuta ya zeri na mafuta* yaliyotengenezwa kwa njia ya pekee kwa mchanganyiko wa vikolezo mbalimbali.+ Isitoshe, waliwasha moto mkubwa isivyo kawaida kwa ajili yake.*
-
-
Yeremia 34:4, 5Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
4 Hata hivyo, sikia neno la Yehova, ewe Mfalme Sedekia wa Yuda, ‘Yehova anasema hivi kukuhusu wewe: “Hutakufa kwa upanga. 5 Utakufa kwa amani,+ nao watakufanyia sherehe ya kufukiza manukato kama walivyowafanyia baba zako, wafalme wa zamani waliokutangulia, nao watakuombolezea wakisema, ‘Ole, ewe bwana!’ kwa maana ‘nimelisema neno hilo,’ asema Yehova.”’”’”
-