Baraka Isiyotazamiwa
✔ Katika nchi moja ya Afrika, jeuri ilitokea kwa ghafula siku ambayo kusanyiko la wilaya la mashahidi wa Yehova lilipomalizika. Aliporudi nyumbani, Shahidi mpya, ambaye hapo kwanza alikuwa wa chama cha kisiasa kilichoanza machafuko hayo, alikuta askari na baraza ya mahali pake wakimngojea. Ulizo lilikuwa, Yeye alikuwa amekuwa akifanya nini wakati wa uasi? Akawaambia kwamba alikuwa amehudhuria kusanyiko la mashahidi wa Yehova. Lakini isitoshe. Walitaka uhakikisho. Askari wakiwa wanafuatana naye, Shahidi huyo akaruhusiwa atoe programu yake ya kusanyiko. Programu yote iliposomwa, jumbe (chifu) akamtangaza Shahidi kuwa asiye na hatia na hata akamtia moyo aendelee na utendaji wake wa kuhubiri. Watu wa kijiji wakashangazwa na jambo hili, wakisema hivi; “Mungu unayeomba ndiye Mungu aliye hai!” Lo! Shahidi huyu alikuwa mwenye shukrani kadiri gani kwa kuwa alikuwa amehudhuria kusanyiko!