Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 8/01 uku. 1
  • Nyinyi Ni “Tamasha”!

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Nyinyi Ni “Tamasha”!
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2001
  • Habari Zinazolingana
  • Wakristo Walioteswa—“Tamasha kwa Dunia”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Malaika—“Roho kwa Ajili ya Utumishi wa Watu Wote”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Malaika—Jinsi Wanavyohusika Katika Maisha Yetu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
  • Waige Malaika Waaminifu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2025
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2001
km 8/01 uku. 1

Nyinyi Ni “Tamasha”!

1 Mtume Paulo aliandika hivi: “Tumekuwa tamasha mbele ya ulimwengu wote, mbele ya malaika na watu.” (1 Kor. 4:9, Biblia Habari Njema) Hiyo yamaanisha nini, na yaathirije huduma yetu leo?

2 Yaelekea usemi “tamasha” ulimkumbusha Mkorintho tukio la mwisho la mashindano ya kupigana ya Waroma ambayo watu waliohukumiwa walisimamishwa mbele ya maelfu ya watazamaji kabla ya kuuawa kikatili. Vivyo hivyo, watazamaji wengi sana—wanadamu na malaika—walitazama mateso ambayo Wakristo wa karne ya kwanza walipata kwa kuhubiri Ufalme. (Ebr. 10:32, 33) Uaminifu wao uliathiri watazamaji wengi, kama vile uvumilivu wetu unavyotazamwa kana kwamba ni katika uwanja wa michezo wa kisasa. Sisi ni tamasha kwa akina nani?

3 Kwa Ulimwengu na kwa Watu: Nyakati nyingine vyombo vya habari huripoti kuhusu utendaji wa watu wa Yehova. Ijapokuwa sisi huthamini ripoti nzuri ambazo ni za kweli na zisizo na ubaguzi kuhusu kazi yetu, pia sisi hutazamia ripoti mbaya zisambazwe na wachongezi wetu mara kwa mara. Hata hivyo, lazima twendelee kujipendekeza wenyewe kuwa wahudumu wa Mungu “kupitia ripoti mbaya na ripoti njema.” (2 Kor. 6:4, 8) Watazamaji wenye mioyo minyofu huona wazi kwamba sisi ndio wanafunzi wa kweli wa Yesu Kristo.

4 Kwa Malaika: Pia viumbe wa kiroho hututazama. Ibilisi na malaika zake hututazama—lakini kwa “hasira kubwa,” wakitafuta kuzuia “kazi ya kutoa ushahidi kuhusu Yesu.” (Ufu. 12:9, 12, 17) Malaika waaminifu wa Mungu hutazama na kufurahia wakati ambapo hata mtenda-dhambi mmoja tu anatubu. (Luka 15:10) Twapaswa kuimarishwa kujua kwamba malaika huiona huduma yetu kuwa kazi ya uharaka zaidi, yenye kunufaisha inayofanywa duniani leo!—Ufu. 14:6, 7.

5 Unapopatwa na upinzani au unapofikiri kwamba huduma yako haina matokeo, kumbuka kwamba unatazamwa na ulimwengu wote. Uvumilivu wako waonyesha jinsi ulivyo mwaminifu. Mwishowe, ‘pigano lako bora la imani’ litakusaidia ‘ushike imara uhai udumuo milele.’—1 Tim. 6:12.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki