Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 10/15 kur. 2-3
  • Jinsi ya Kufikia Mioyo ya Wale Tunaowafundisha

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Jinsi ya Kufikia Mioyo ya Wale Tunaowafundisha
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2015
  • Habari Zinazolingana
  • Jitahidi Kugusa Moyo
    Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
  • Sitawisha Ustadi wa Kufundisha
    Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
  • Unapofundisha, Fikia Moyo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Kupendezwa na Wengine
    Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2015
km 10/15 kur. 2-3

Jinsi ya Kufikia Mioyo ya Wale Tunaowafundisha

1. Ufundishaji wa Yesu ulikuwa na matokeo gani katika mioyo ya wasikilizaji wake?

1 Yesu Kristo alifikia mioyo ya wasikilizaji wake. Katika pindi moja, mioyo ya wanafunzi wake ilikuwa “ikiwaka” baada ya kuwafafanulia vizuri Maandiko. (Luka 24:32) Kwa kuwa utii kwa Mungu unapaswa kutoka moyoni, tunaweza kuchochea jinsi gani mioyo ya wale tunaowafundisha ili wafanye mabadiliko katika maisha yao?—Rom. 6:17.

2. Kuwa mwenye busara na utambuzi kutakusaidiaje kufikia moyo wa mtu?

2 Uwe Mwenye Busara na Utambuzi: Kwa kawaida watu wengi hawachochewi kuchukua hatua kwa kuambiwa tu jambo linalofaa na lisilofaa. Kwa kweli, ikiwa tunashutumu mafundisho ya dini zao kwa kutumia maandiko mengi, huenda jambo hilo likawafanya wasipendezwe na mafundisho yetu. Ili kumchochea mtu, kwanza unahitaji kutambua sababu zinazomfanya aamini na kutenda jambo fulani. Tukiuliza maswali ya maoni kwa busara tutamchochea aeleze maoni yake kutoka moyoni. (Met. 20:5) Hilo litakusaidia kuchagua habari kutoka kwenye Neno la Mungu itakayogusa hisia zake. Kwa hiyo, tunapaswa kupendezwa nao kibinafsi na kuwa na subira. (Met. 25:15) Unapaswa kukumbuka kwamba kila mmoja hufanya maendeleo ya kiroho kwa kiwango tofauti. Ruhusu muda upite ili roho takatifu ya Yehova ibadili fikira na matendo yao.—Marko 4:26-29.

3. Tunaweza kuwasaidiaje wale tunaowafundisha kusitawisha sifa nzuri?

3 Wasaidie Wasitawishe Sifa Nzuri: Masimulizi ya Biblia yanayoeleza kuhusu upendo na wema wa Yehova yanaweza kuwasaidia wale tunaowafundisha kusitawisha sifa nzuri. Tunaweza kutumia andiko la Zaburi 139:1-4 au Luka 12:6, 7 kuwaonyesha jinsi Mungu anavyopendezwa kibinafsi na kila mmoja wetu. Watu wanapoanza kuthamini fadhili zisizostahiliwa za Yehova, upendo na ujitoaji wao kwa Mungu unaongezeka. (Rom. 5:6-8; 1 Yoh. 4:19) Pia, wanapojifunza kwamba matendo yao yanaweza kumfurahisha au kumhuzunisha Yehova, huenda wakachochewa kutenda katika njia itakayomfurahisha na kumheshimu.—Zab. 78:40, 41; Met. 23:15.

4. Tunapowafundisha watu katika huduma, tunawezaje kuheshimu uhuru wao wa kuamua?

4 Yehova hamlazimishi mtu yeyote kutii sheria zake. Badala yake, anawasihi watu kwa kuwaonyesha faida ya kufuata ushauri wake. (Isa. 48:17, 18) Tunamwiga Yehova kwa kuwafundisha watu katika njia inayowasaidia wafanye maamuzi yao binafsi. Watu wanapoamua wenyewe kufanya mabadiliko fulani maishani, maamuzi yao hudumu. (Rom. 12:2) Hilo linawasaidia pia kumkaribia Yehova, “mchunguzaji wa mioyo.”—Met. 17:3.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki