-
Walevi Wa Kiroho—Wao Ni Nani?Mnara wa Mlinzi—1991 | Juni 1
-
-
20, 21. Mashahidi wa Yehova hupiga mbiu habari gani bila kukoma, lakini viongozi wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo hukataa kufanya nini?
20 Unabii unasema hivi juu ya watu kama hao: “Ambao aliwaambia, Hii ndiyo raha yenu, mpeni raha yeye aliyechoka; huku ndiko kuburudika; lakini hawakutaka kusikia. Kwa sababu hiyo neno la BWANA [Yehova, NW] kwao litakuwa hivi, amri juu ya amri, amri juu ya amri; kanuni juu ya kanuni, kanuni juu ya kanuni; huku kidogo na huku kidogo; ili waende na kuanguka nyuma, na kuvunjwa, na kunaswa, na kuchukuliwa.”—Isaya 28:12, 13.
-
-
Walevi Wa Kiroho—Wao Ni Nani?Mnara wa Mlinzi—1991 | Juni 1
-
-
22. Yehova ajulisha viongozi wa kidini jambo gani?
22 Kwa sababu hiyo, maneno ya Isaya ya kiunabii yajulisha makasisi kwamba Yehova hatanena sikuzote kwa njia ya Mashahidi Wake wasio na dhara. Karibuni, Yehova atatekeleza “amri [yake] juu ya amri, kanuni juu ya kanuni,” na matokeo yatakuwa msiba mkuu kwa Jumuiya ya Wakristo. Viongozi wayo wa kidini na makundi yao ‘watavunjwa, na kunaswa, na kuchukuliwa.’ Ndiyo, kama Yerusalemu wa kale, mifumo ya kidini ya Jumuiya ya Wakristo itaharibiwa kabisa kabisa. Hiyo itakuwa tukio lisilotazamiwa, lenye kushtua kama nini! Nalo ni tokeo lenye kuogofya kama nini kwa sababu makasisi hupendelea ulevi wa kiroho, badala ya vikumbusha vya Yehova!
-