Wimbo 221
Vijana! Fuateni Mfano wa Imani Yao
1. Kijana Samweli kaenda Shilo
Atumike hekaluni mwa Mungu.
Akawa nabii wa Israeli,
Munadhiri, kaheshimu Yehova.
Wana wa Eli wakawa wabaya.
Je! Samweli kijana apotoshwe?
La, ni mwaminifu; naye atii.
Naye hakumwacha Yehova kamwe.
2. Kijana Timotheo, alijua
Maandiko, ili awe muzee.
Alitenda mambo aliyofunzwa.
Alitaka kubaki mwaminifu.
Akawa na sifa njema kundini,
Alipendekezwa bila kupingwa.
Kapendelewa kwenda na Paulo;
Na alikuwa baraka kwa wote.
3. Kisichana Mwisraeli na yeye
Aliamini Yehova kabisa.
Ajapotekwa, kawa mwaminifu;
Aliwasaidia wengineo.
Kajulisha mukeye Naamani:
’Nabii wa Yehova anaponya.’
Naamani akamusikiliza.
Akabarikiwa kwa tendo hilo.
4. Nanyi ndugu, nanyi dada wachanga,
Fuateni mifano hiyo myema.
Tunayo amana “siku za mwisho.”
Yehova amechagua wajumbe.
Vijana, mwingie, mupige vita
Pamoja na watumishi wa Mungu
Tutangaze onyo na sifa yake
Na kuthawabishwa hapo mwishoni.