BIBLIOTEKE YA KU ENTERNETE Watchtower
Watchtower
BIBLIOTEKE YA KU ENTERNETE
Swahili (Katanga)
  • BIBLE
  • BITABU
  • MA RENION
  • w25 Novembre pp. 2-7
  • Endelea kuwa na furaa ata kama unazeka

Akuna video nju ya iyi selection.

Pardon, kurikuwa erreur mu chargement ya video.

  • Endelea kuwa na furaa ata kama unazeka
  • Munara ya Mulinzi Inatangaza Ufalme ya Jeova (ya kufunda)—2025
  • Sous-titres
  • Ya kufanana na iyi
  • AINA TEKETEKE KWENDELEA KUWA NA FURAA SAA UKO NAZEKA
  • MAMBO YA KUFANYA NJU YA KWENDELEA KUWA NA FURAA
  • NAMNA BENGINE BANEZI KUSAIDIA
  • Jeova anezi kutusaidia tukuwe na “furaa ya bya kweri”
    Munara ya Mulinzi Inatangaza Ufalme ya Jeova (ya kufunda)—2025
Munara ya Mulinzi Inatangaza Ufalme ya Jeova (ya kufunda)—2025
w25 Novembre pp. 2-7

ABARI YA KUFUNDA YA 44

MWIMBO 138 Uzuri wa Kichwa Yenye Imvi

Endelea kuwa na furaa ata kama unazeka

‘Wakati ya buzee . . . batachipuka.’​—ZB. 92:14.

MU KIFUPI

Ni kintu kya lazima ku bale bashakuzeka bachunge furaa yabo, na namna banezi kufanya vile.

1-2. Jeova anaonaka je bakristo baminifu bale bashakuzeka? (Zaburi 92:12-14; angaria na foto ya pa couverture.)

MU MAFASHI ingine ya mu dunia bantu banaonaka asema kuzeka ni kintu kya eshima sana, lakini mu mafashi ingine bantu banafanyaka nguvu yabo yote nju bashionekane sa bashakuzeka. Kwa mufano, kama banaona ka nywele ka mweupe kananza banakakata mala moya. Lakini ata bafanye je batafikia tu paka kuzeka.

2 Jeova anaonaka je batumishi bake bale bashakuzeka? (Mez. 16:31) Anabafananisha na michi ya muzuri sana. (Soma Zaburi 92:12-14.) Nju ya nini? Mala mingi michi ile ishakukomea sana inekalaka muzuri sana nju inekalaka na mayani ya mingi na ma fleur ya mingi. Mu michi ya kushangaisha sana, muko ile banaita cerisier du Japon. Kuko ma cerisier du Japon ile ishakupitisha miaka 1 000, ile inaonekanaka ya muzuri sana. Sa vile ile michi, banduku na badada baminifu bale bashakuzeka beko ba maana sana kwa Jeova. Jeova ashionake tu vile bashakuzeka, lakini anaonaka njo ma roo yabo. Jeova anapendaka sana masifa yabo ya muzuri, namna banamutumikia miaka mingi, na namna banaendelea kubakia baminifu mu wakati ya muzuri na mu wakati ya magumu.

Bibi na bwana bale basha kuzeka banaikala pa kichi inje pa fashi pale peko ma cerisier ya mingi ya muzuri.

Saa tu michi ile ishakufanya miaka mingi inekalaka ya muzuri na inaendeleaka kuchipuka, banduku na badada baminifu bale bashakuzeka banaendelea kuwa ba maana (Angari paragrafe 2)


3. Leta mufano ile inaonesha vile Jeova aritumikishaka batumishi bake bale bashakuzeka nju bafanye kaji ya lazima.

3 Jeova anendeleaka kutuona ba maana ata kama tushakuzeka.a Mala mingi, Jeova anatumikishaka bantu bale bashakuzeka nju bafanye kaji ya maana sana. Kwa mufano, Sara arikuwaka ashakuzeka sana saa Jeova arimwambia kama atapata mutoto, na kama kupitia ule mutoto atakuwa mama wa taifa munene sana na kambo yake ya Masiya. (Mwa. 17:15-19) Moïse arikuwa ashakukomea sana saa Jeova arimupachia kaji ya kutosha batoto ya Israel mu Egypte. (Kut. 7:6, 7) Mutume Yohana na ye arikuwa ashakuzeka saa Jeova arimupachia kaji ya kwanjika bitabu bi 5 bya mu Bible.

4. Kupatana na Mezali 15:15, ni nini njo inezi kusaidia bale bashakuzeka bavumilie magumu ile beko napata? (Angaria na foto.)

4 Buzee bunakuyaka na magumu ya mingi. Dada moya ule ashakuzeka arisemaka ivi mu mizaa: “Kukomea aina teketeke.” Lakini kuwa na furaab kutasaidia bale bashakuzeka bavumilie magumu ile banapataka nju ya buzee. (Soma Mezali 15:15.) Mu iyi abari, tutaona mambo ile bale bashakuzeka banezi kufanya nju baendelee kuwa na furaa. Tutaona tena kile bengine banezi kufanya nju ya kusaidia banduku na badada bale bashakuzeka ba mu makutaniko yabo. Tuone mbele nju ya nini inekalaka nguvu kwa muntu kwendelea kuwa na furaa saa eko nazeka.

Bale babibi na bwana basha kubambana ku mikono beko na furaa na basha kushimama chini ya cerisier.

Kwendelea kuwa na furaa kutasaidia bale bashakuzeka kuvumilia magumu ya buzee (Angaria paragrafe 4)


AINA TEKETEKE KWENDELEA KUWA NA FURAA SAA UKO NAZEKA

5. Ni nini njo inezi kufanya bantu bengine bale bashakuzeka bajishikie mubaya?

5 Saa uko nazeka, ni nini njo inezi kukufanya ujishikie mubaya? Pengine ni nju autaweza kufanya bile urianzaka kufanya. Uko napenda wendelee kuwa na santé ya muzuri sa pale urikuwaka ungariki kiyana. (Muh. 7:10) Dada Ruby anajishikiaka saa moya kuwa dekurajé. Anasema ivi: “Saa moya ata kuvwala manguo ni nguvu nju ya maumivu ile minashikiaka na nju minashindaka kushimama muzuri. Na bintu bya teketeke sa vile, kuvwala shosete binanikuiaka paka nguvu. Mikono yangu inaniumaka, na binekalaka nguvu kwangu kufanya ata makaji ya kiloko.” Nduku Harold aritumikaka nzamani ku Betele. Anasema ivi: “Saa moya minashikiaka mubaya nju shiweze tena kufanya mambo ile mirianzaka kupenda kufanya. Mirikuwaka na nguvu sana saa nirikuwaka kiyana. Miripendaka sana kucheza base-ball. Bantu barianzaka kusema, ‘mumupachie Harold balon nju atatusaidia kuwina.’ Lakini leo shiyuwe ata kama minezi kuweza kutupa balon.”

6. a) Ni mambo kani ingine ile inezi kudekurajé bale bashakuzeka? b) Ni nini inezi kusaidia muntu ule ashakuzeka ayuwe kama ataacha ao ataendelea kubulula motoka, nkinga ao moto? (Soma abari “Niache kubulula?”)

6 Pengine uko najishikia mubaya nju auweze tena kurifanshia mambo ingine we moya. Pengine uko na lazima ya muntu wa kukusaidia kufanya mambo ingine, ao saa unapenda kutoka uko na lazima mutoto yako akusindikize. Ao pengine unapotesha furaa yako nju santé yako aina tena muzuri ao mancho yako aione tena muzuri nju uweze kwenda mafashi ingine we moya ao nju uweze kutembesha motoka, nkinga, ao moto. Bile byote binafanyaka muntu arishikie mubaya sana! Ata kama auweze tena kufanya mambo ile urianzaka kufanya we moya, kumbuka asema uko paka wa maana kwa Jeova na kwa bantu bengine. Na tunezi kuwa sire asema Jeova eko nakomprandre vile tuko najishikia. Jeova anayuwa vile tunamupenda sana na vile tunapenda sana banduku na badada yetu. Na ile njo inafanya tukuwe ba maana sana kwake.​—1 Sa. 16:7.

7. Ni nini inezi kusaidia bale beko nashikia mubaya nju beko nawaza asema mwisho itafika na bashakufwa?

7 Pengine unashikia mubaya nju unawaza asema mwisho itafika na ushakufwa. Kama unajishikia vile, ona kile kinezi kukusaidia: Kumbuka asema kuko kile kiko namusukuma Jeova achunge, mbele ya kuleta mwisho. (Isa. 30:18) Sasa nju ya nini Jeova eko nachunga? Ni nju ya kusaidia bantu ba mingi bapate okazion ya kumuyuwa na kumutumikia. (2 Pe. 3:9) Kama unajishikia kuwa dekurajé, kumbuka asema kuchunga kwa Jeova kutasaidia bantu ba mingi bamuyuwe mbele mwisho ifike. Pengine mu bale bantu munezi kuwa ata bantu ba mu famiye yako.

8. Malari ao maumivu inezi kusukuma muntu ule ashakuzeka afanye nini?

8 Ata tukuwe na miaka ngapi, kama atujishikie muzuri, saa moya tunafanyaka ao kusema mambo ile atukupashwe kufanya ao kusema. (Muh. 7:7; Yak. 3:2) Kwa mufano, saa Job arikuwa mu mateso, arisema misemo ile aina mu njia. (Yob. 6:1-3) Kintu kingine kile kinezi kufanya muntu aseme mambo ile ashikupende kusema, inezi kuwa malari ao efé ya madawa ile eko nakunywa. Lakini ata kama tushakuzeka ao tuko malari, aitakuwa muzuri tuseme bengine mubaya ao kuwaza asema banapashwa kutufanshia kila kintu. Na kama tunakumbuka asema turimusema muntu mubaya, tumulombe buluma.​—Mt. 5:23, 24.

MAMBO YA KUFANYA NJU YA KWENDELEA KUWA NA FURAA

Muchi ya cerisier ya muzuri; tumafoto tuloko tunaonesha mambo ile banduku na badada bale basha kuzeka beko nafanya nju ya kwendelea kuwa na furaa. Ile mambo banaizungumuzia mu paragrafe 9-13.

Namna kani unezi kwendelea kuwa na furaa ata kama uko na magumu ya buzee? (Angaria paragrafe 9-13)


9. Nju ya nini ni muzuri uichike bengine bakusaidie? (Angaria na foto.)

9 Ichika bengine bakusaidie. (Gal. 6:2) Ku mwanzo, ni nguvu kufanya vile. Dada Gretl anasema ivi: “Saa moya, binekalaka nguvu kwangu kwichika bengine banisaidie nju minawazaka asema minezi kuwa muziko kwabo. Irinibeba wakati ya mingi nju ya kushanjé mawazo yangu na nichike asema niko na lazima bengine banisaidie.” Kumbuka asema bengine batakuwa na furaa kama unechika bakusaidie. (Mdo. 20:35) Na weye utafurai kuona vile bantu bengine banakupenda na kukwangaikia sana.

Dada wa kuzeka anabamba ku mukono ya dada kiyana saa beko nauza bintu mu nsoko.

(Angaria paragrafe 9)


10. Nju ya nini ni muzuri kukumbuka kusema merci? (Angaria na mafoto.)

10 Sema merci. (Kol. 3:15; 1 Te. 5:18) Saa bengine banatufanshia kintu kya muzuri, tunashikiaka muzuri. Lakini saa moya tunasabwaka kusema merci. Saa muntu anakufanshia kintu kya muzuri, ni muzuri kufurai na kusema merci. Kufanya vile kutasaidia barafiki yetu baone asema tunabeba na valere mambo ile beko natufanshia. Dada Leah anasaidiaka bantu ba kuzeka bale beko ku Betele. Anasema ivi: “Dada moya wa kuzeka ule minangaikiaka, ananianjikiaka nju ya kunipikia merci. Ashinianjikiake mambo ya mingi, lakini minaifuraiaka. Minapendaka kusoma bile ananianjikiaka na binanipachiaka furaa ya kuyuwa asema anafuraiaka bile minamufanshiaka.”

Dada wa kuzeka eko nanjika nju ya kupika merci.

(Angaria paragrafe 10)


11. Unezi kufanya nini nju ya kusaidia bengine? (Angaria na mafoto.)

11 Fanya kile utaweza nju ya kusaidia bengine. Kama unatumikisha wakati yako na nguvu yako nju ya kusaidia bengine, unezi ata kusabu magumu yako. Bantu bale bashakuzeka beko sa bitabu bile biko nafundisha mambo ya maana. Lakini, kama bantu abasome bile bitabu, abatafunda mambo ya muzuri ile ikwamo. Njo pamoya na weye, babiyana abatafunda mambo ya mingi kutoka kwako kama ausumburie nabo na kubaambia mambo ile unayuwa. Ubaulize maulizo na ubashikie. Ubaoneshe asema kufwata mambo ile Jeova anatulomba njo kutabaletea tu furaa. Kusema tu bya kweri, kwankurajé biyana kutakuletea na weye furaa.​—Zb. 71:18.

Nduku wa kuzeka eko nashikia saa nduku kiyana eko namwambia mambo yake.

(Angaria paragrafe 11)


12. Kupatana na Isaya 46:4, Jeova analaka kufanshia nini bale bashakuzeka? (Angaria na mafoto.)

12 Umulombe Jeova akupachie nguvu. Ata kama saa moya unashikia maungu inachoka ao unachoka mu akiri, kumbuka asema Jeova yeye “ashichokake na nguvu aimwishake.” (Isa. 40:28) Jeova anatumikishaka je nguvu yake ile aina na mwisho? Anaitumikishaka mu ma namna ya kwachana-achana. Namna ingine ile anaitumikishaka ni kupachia nguvu batumishi bake baminifu bale bashakuzeka. (Isa. 40:29-31) Kusema kweri, Jeova ye moya analaka asema atakusaidia. (Soma Isaya 46:4.) Na kila shiku Jeova anafanyaka bile analaka. (Yos. 23:14; Isa. 55:10, 11) Saa unasali kwa Jeova, na kuona vile anakupachia mambo ile uko nayo lazima, utayuwa asema anakupenda sana. Na kuyuwa vile kutakusaidia ukuwe na furaa.

Nduku wa kuzeka eko nasali.

(Angaria paragrafe 12)


13. Kupatana na 2 Wakorinto 4:16-18, tunapashwa kukumbuka nini? (Angaria na mafoto.)

13 Kumbuka asema autendelea kuwa muzee. Saa unakumbuka asema magumu ile uko napata itaishaka, utaweza kuivumilia. Bible inatulaka asema buzee na malari bitaishaka. (Yob. 33:25; Isa. 33:24) Kumbuka asema bizuri aina bile bishakupita, lakini ni bile biko nakuchunga ku mbele. Kuyuwa vile kutakuletea furaa. (Soma 2 Wakorinto 4:16-18.) Sasa, shiye bengine tunezi kufanya nini nju ya kusaidia bale bashakuzeka?

Dada wa kuzeka eko mu kankinga ka ba bilema na eko nasoma Bible. Eko najiwazia vile atakuwa kiyana mu paradi na vile ashitakuwa tena na lazima ya kale kankinga.

(Angaria paragrafe 13)


NAMNA BENGINE BANEZI KUSAIDIA

14. Nju ya nini ni muzuri kutembelea na kuita bale bashakuzeka?

14 Wanze kuita na kutembelea banduku na badada bale bashakuzeka. (Ebr. 13:16) Bale bashakuzeka banezi kujishikia mubaya nju beko napitisha wakati ya mingi bo benyewe. Nduku Camille anabakiaka tu ku nyumba. Anasema ivi: “Saa moya minashikiaka mubaya na minashikiaka makari nju shiwezi kutoka ku nyumba na shina na bya mingi bya kufanya.” Saa tunatembelea bale bashakuzeka, tunaonesha asema beko ba maana kwetu na tunabapenda. Pengine, kuko wakati turipendaka kuita ao kutembelea muntu ule ashakuzeka, lakini atukufanyake vile. Kusemna tu bya kweri, shiye bote tuko na mambo mingi ya kufanya. Sasa ni nini njo inezi kutusaidia ‘kuyuwa mambo ya lazima sana?’ Nju mu mambo ya lazima sana muko na kutembelea bale bashakuzeka. (Flp. 1:10) Kintu kile kinezi kukusaidia, ni kwanjika manjina ya bale bashakuzeka ba mu kutaniko yako, na kwanjika shiku ile utabaita ao kubatumia message. Na ni muzuri tena kupanga shiku ile utabatembelea nju kama aufanye vile unezi kusabu.

15. Ni mambo kani biyana na bale bashakukomea banezi kufanya pamoya?

15 Kama uko kiyana, unezi kujiuliza ni mambo kani unezi kusumburia na muntu ule ashakuzeka ao ni mambo kani munezi kufanya pamoya. Lakini ushijiangaishe sana. Ukuwe tu rafiki muzuri. (Mez. 17:17) Mbele na kisha renion sumburia na bale bashakuzeka ba mu kutaniko yako. Pengine unezi kubauliza nju ya mandiko ile banapendaka ao kubauliza nju ya mambo ya kuchekesha ile barifanyaka saa barikuwaka bakingariki batoto. Unezi ata kufwata pamoya nabo emision ya JW Télédiffusion. Unezi ata kubasaidia kufanya mambo ile abataweza kufanya bo benyewe, sa vile kutelesharjé bitabu mu telefone ao mu tablete yabo. Dada Carol anasema ivi: “Bile unapendaka kufanya ubifanye pamoya na muntu ule ashakuzeka. Ata kama nishakuzeka, minapendaka kufanya mambo ile minafuraiaka. Minapendaka kwenda kuuza bintu, kurya pamoya na barafiki, na kupitisha wakati pamoya nju ya kujifuraisha.” Dada Maira anasema ivi: “Niko na rafiki yangu ule eko na miaka 90. Ananipita ku miaka 57. Minasabwaka ata kama ashakunipita ku ile miaka yote nju tunachekaka pamoya na tunangariaka mafilme pamoya. Na wakati tunapata magumu, kila muntu anatafutaka mashauri kwa mwenzake.”

16. Nju ya nini ni muzuri kusindikiza bale bashakuzeka ku opitale?

16 Ubasindikize ku opitale. Ni muzuri kubapeleka ku opitale, lakini ni muzuri tena kwikala nabo pamoya na kuona kama badoktere beko nabatendea muzuri. (Isa. 1:17) Unezi kusaidia muntu ule ashakuzeka saa uko nanjika mambo ile doktere eko namuonesha. Dada Ruth ashakuzeka. Anasema ivi: “Mala mingi saa minenda ku opitale mi moya, doktere ashichikake bile niko namwambia. Saa moya badoktere banasemaka ivi: ‘Uko nawaza sa uko malari lakini auna malari.’ Lakini saa muntu mwingine ananipeleka, doktere ananiangaikiaka muzuri. Minapikia merci banduku na badada bote bale banatumikishaka wakati yabo nju ya kunipeleka.”

17. Unezi kufanya maubiri ya je pamoya na bale bashakuzeka?

17 Ubiri pamoya nabo. Pengine banduku na badada bale bashakuzeka abana na nguvu ya kuubiri nyumba na nyumba. Pengine unezi kulomba dada ule ashakuzeka aubiri na weye ku prezantware. Unezi ata kumuletea kichi nju ekale mpembeni ya prezantware. Unezi ata kwenda naye kwa muntu ule munafundaka naye Bible, ao unezi ata kwambia ule muntu akuye kwa nduku ao kwa dada ule ashakuzeka nju mufundie kule. Bazee banezi kupanga ata kufanshia ma renion ya maubiri kwa nduku ao dada ule ashakuzeka. Nju kufanya vile kutamusaidia na yeye ashikose ile ma renion. Jeova anafuraiaka mambo yote ile tunafanyaka nju ya kuonesha asema tunapenda na kweshimia banduku na badada bale bashakuzeka.​—Mez. 3:27; Ro. 12:10.

18. Tutafunda nini mu abari ile iko nafwata?

18 Iyi abari inatukumbusha asema Jeova anapendaka batumishi bake bale bashakuzeka na anabaonaka kuwa ba valere. Na njo vile shiye bote mu kutaniko tunabaonaka! Buzee abuna teketeke, lakini Jeova atakusaidia wendelee kuwa na furaa. (Zb. 37:25) Na inafuraisha kuyuwa asema mashiku ya muzuri aina ile uriacha ku mukongo, lakini ni ile iko nakuchunga ku mbele! Kuko banduku na badada bale beko na magumu ingine nju banapashwa kwangaikia muntu wa mu famiye ule ashakuzeka, ao kwangaikia mutoto ao rafiki ule eko malari. Banezi kufanya nini nju baendelee kuwa na furaa? Tutapata jibu ya ile ulizo mu abari ile iko nafwata.

UTAJIBU JE?

  • Ni mambo kani ile inezi kufanya banduku na badada bale bashakuzeka bapoteshe furaa yabo?

  • Bale bashakuzeka banezi kufanya nini nju baendelee kuwa na furaa?

  • Tunezi kufanya mambo kani nju ya kusaidia bale bashakuzeka ba mu kutaniko yetu?

MWIMBO 30 Baba Yangu, Mungu Wangu, na Rafiki Yangu

a Angaria ku jw.org na ku JW Library® video Wakristo Wenye Kuzeeka Ni wa Maana.

b ESPLIKASION YA MANENO FULANI: Furaa ni kipande kya ntunda ya roo ya Mungu. (Gal. 5:22) Nju tupate furaa ya bya kweri, tunapashwa kuwa na burafiki bwa karibu sana pamoya na Jeova.

    Swahili (Katanga) Publications (2020-2026)
    Toka
    Ingia
    • Swahili (Katanga)
    • Partajé
    • Preferanse
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni ya kutumikisha
    • Règles de confidentialité
    • Paramètres de confidentialité
    • JW.ORG
    • Ingia
    Partajé