ABARI YA KUFUNDA YA 43
MWIMBO 41 Tafazali, Sikia Sala Yangu
Kumbuka kusali nju ya bengine
“Kila muntu asali nju ya mwenzake. . . Sala ya kumuriria Mungu ya muntu mwaminifu iko na nguvu sana.”—YAK. 5:16.
MU KIFUPI
Nju ya nini ni muzuri kusali nju ya bengine na namna ya kufanya vile.
1. Tunayuwa je asema ma sala yetu iko ya maana sana kwa Jeova?
SALA ni kado ya muzuri sana. Waza ata weye, kuko ma kaji ile Jeova anapachia bamalaika bafanye. (Zb. 91:11.) Na kuko ma kaji ya maana sana ile arimupachia mutoto yake afanye. (Mt. 28:18) Sasa tuseme nini nju ya kaji ya kushikia sala? Ile ni kaji Jeova anafanyaka ye moya na ashiipachiake muntu mwingine. Jeova njo ‘ule anashikiaka sala,’ ye mwenyewe anatushikiaka.—Zb. 65:2.
2. Paul arisali nju ya bengine, mufano yake inezi kutufundisha nini?
2 Ata kama tunapashwa kumwambia Jeova nju ya mambo yetu, tunapashwa tena kusali nju ya bengine. Njo vile na Paul arifanyaka. Kwa mufano, arianjikia kutaniko ya Efeso ivi: “Minendelea kumitaya mu ma sala yangu.” (Efe. 1:16) Na kuko saa Paul arisali nju ya muntu moya-moya. Kwa mufano arimwambia Timothée ivi: “Minamupikia Mungu merci, . . . na mishiache ata kiloko kukukumbuka mu ma sala yangu ya kumuriria Mungu bushiku na mu yuwa.” (2 Ti. 1:3) Paul ashikukose bya kusali, arikuwa na ye na mambo yake ile irianzaka kumwangaisha. (2 Ko. 11:23; 12:7, 8) Ata vile, aribeba na wakati ya kusali nju ya bengine.
3. Nju ya nini tunezi kusabu kusali nju ya bengine?
3 Saa moya tunezi kusabu kusali nju ya bengine. Nju ya nini? Dada Sabrinaa anonesha kintu kimoya kile kinezi kufanya tusabu kusali nju ya bengine. Anasema ivi: “Mu iyi dunia kuko bintu bya mingi bya kufanya. Tunezi kwanza kuwaza sana nju ya mambo ile tuko nayo, na ile inezi kufanya tusali tu nju ya mambo yetu shiye benyewe.” Eske bya vile binakufikiaka na weye? Kama ni vile, iyi abari itakusaidia sana. (1) Itaonesha nju ya nini ni kintu kya lazima kusali nju ya bengine na (2) mambo ile unezi kufanya nju uyuwe namna ya kufanya vile.
NJU YA NINI TUSALI NJU YA BENGINE?
4-5. Namna kani sala ile tunafanya nju ya bengine “iko na nguvu sana”? (Yakobo 5:16)
4 Sala ile tunafanya nju ya bengine “iko na nguvu sana.” (Soma Yakobo 5:16.) Kusali nju ya bengine kunezi kusaidia? Kunezi kusaidia. Yesu ariyuwaka asema Petro atafikia kumukana, njo maana arimwambiaka ivi: “Mirimuriria Mungu nju yako nju imani yako ishipole.” (Lu. 22:32) Paul naye ariyuwaka asema sala iko na nguvu. Saa barimubambaka pashipo mambo na kumufunga mu prizon ya Rome, arimwanjikiaka Filemon ivi: “Niko na kitumaini kama kupitia ma sala yenu batanifungula na mitarudia tena kwenu.” (Flm. 22) Na njo vile mambo irikuwa, kisha wakati kiloko barimufungula Paul na arianza tena kuubiri.
5 Lakini ile aioneshe asema kama tunasali, Jeova anapashwa tu kufanya paka bile tunamulomba. Jeova anayuwa muzuri mambo ile batumishi bake beko namulomba, na saa moya anekalaka eko najibu ku bile banamulomba. Kuyuwa vile kutatusukuma tusali kwa Jeova na roo moya na twache mambo mu mikono yake.—Zb. 37:5; 2 Ko. 1:11.
6. Kusali nju ya bengine kunezi kutufanya tujishikie je nju yabo? (1 Petro 3:8)
6 Kusali nju ya bengine kunatusaidia tukuwe na “buluma bwa sana.” (Soma 1 Petro 3:8.) Kushikiria muntu buluma, ni kuyuwa magumu ile eko nayo na kupenda kumutosha mu ile magumu. (Mk. 1:40, 41) Michael muzee moya anasema ivi: “Saa niko nasali nju ya magumu ya bengine, minafikiaka kukomprandre muzuri magumu ile beko nayo, na ile inafanyaka nibapende tena sana. Ile inafanya nijione kuwa karibu nabo ata kama pengine bo abayuwe vile.” Richard muzee mwingine naye anasema ivi: “Saa tunasali nju ya muntu mwingine, roo inatusukumaka tupende kufanya kintu nju ya kumusaidia.” Na anaongeza ivi: “Saa tunasaidia muntu ule turisali nju yake, iko sa vile tuko nasaidia kuleta jibu ku sala ile turifanya nju yake.”
7. Namna kani kusali nju ya bengine kunatusaidia tushiweke akiri paka ku magumu yetu? (Wafilipi 2:3, 4) (Angaria na mafoto.)
7 Kusali nju ya bengine kunatusaidia tuyuwe asema aina paka shiye njo tuko na magumu. (Soma Wafilipi 2:3, 4.) Shiye bote tunapataka magumu nju tuko naishi mu dunia ile iko mu mikono ya Shetani. (1 Yo. 5:19; Ufu. 12:12) Kuzobelea kusali nju ya bengine kunatukumbushaka asema “banduku [yetu] ba mu dunia mujima [na bo] beko napata ile mateso moya-moya.” (1 Pe. 5:9) Katherine dada painia anasema ivi: “Kusali nju ya bengine kunanikumbushaka asema na banduku bengine banapataka magumu. Kuyuwa vile kunanisaidia nishiweke akiri yote paka ku magumu yangu.”
Kusali nju ya bengine kunatusaidia tuyuwe asema aina paka shiye njo tuko na magumu (Angaria paragrafe ya 7)d
BEKO NA LAZIMA YA SALA YETU
8. Tunezi kusali nju ya bantu kani.
8 Tutasali nju ya nani? Tunezi kusali nju ya bantu bamingi, kwa mufano: Tunezi kusali nju ya bale beko malari, nju ya batoto bale benzabo beko nabacheka ku masomo, ao nju ya bale beko na magumu ya buzee. Banduku yetu bamingi beko nateswa nju maguvernema iko nabateswa ao nju bantu ba mu famiye yabo beko nabateswa nju ya imani yabo. (Mt. 10:18, 36; Mdo. 12:5) Banduku bengine banapashwa kuacha manyumba yabo nju ya kukimbia mafujo ya politike. Bengine beko nateswa nju ya manvula ya nguvu, mavolkan, bulongo kutetemeka na mambo ingine ya vile. Pengine atuyuwe banduku na badada yetu bote bale beko napata magumu. Lakini saa tunasali nju yabo, tunaonesha asema tunafwata mambo ile Yesu arituoneshaka ya kusema “mupendane.”—Yoh. 13:34.
9. Nju ya nini tunapashwa kusali nju ya bale beko natuongoza mu organizasion ya Jeova, na nju ya nini tunapashwa kusali nju ya babibi yabo?
9 Tunapashwa tena kusali nju ya bale beko natuongoza mu oraganizasion ya Jeova, nikusema kusali nju ya Collège central, na ba assistant babo, ma Comité ya filiale, bale beko nashimamia makaji ku Mabetel, baangalizi ba muzunguko, bazee ba makutaniko na ba assistant. Bale banduku nabo banekalaka na magumu yabo, lakini banatumikaka sana nju yetu. (2 Ko. 12:15) Kwa mufano, Mark mwangalizi moya wa muzunguko anasema ivi: “Kintu kimoya kile kinaniangaishaka sana ni kuwa mbari sana na bazazi yangu. Bashakuzeeka na bote bawiri beko malari-malari. Ata kama dada yangu na bwana yake njo beko nabangaikia, inanyumaka sana kuona asema minezi kufanya tu mambo kiloko nju ya kubasaidia.” Ata kama tunayuwa ao kama atuyuwe magumu ile aba banduku benye banatumikaka sana beko nayo, ni muzuri twendelee kusali nju yabo. (1 Te. 5:12, 13) Tunezi tena kusali nju ya babibi yabo, nju beko nabasaidia sana bendelee na kaji yabo.
10-11. Saa tunasali nju ya banduku na badada bamingi ku mala moya, Jeova anafuraiaka ile sala? Leta mufano.
10 Sa vile turiona, mala mingi tunekalaka tuko nasali nju ya bikunji bya banduku na badada. Kwa mufano, ata kama mu akiri atuyuwe tusali nju ya muntu kani, tunezi kumulomba Jeova asaidie bale beko mu prizon, ao apachie nguvu bale barifisha. Donald, muzee moya anasema ivi: “Tuko na banduku na badada bamingi bale bekonapata magumu, njo pale saa moya tunamulombaka Jeova asaidie bale bote beko mu magumu.”
11 Eske ile ma sala ya vile inamufuraishaka Jeova? Inamufuraishaka! Kusema tu bya kweri, atuyuwe magumu yote ya kila nduku na dada. Njo pale inekalaka muzuri tusali nju ya banduku na badada bote. (Yoh. 17:20; Efe. 6:18) Ma sala ya vile inonesha asema ‘tunapenda banduku bote.’—1 Pe. 2:17.
SAA UKONASALI NJU YA MUNTU MOYA-MOYA
12. Kuangaria muzuri kutakusaidia je uyuwe bantu bale utataya mu sala yako na mambo ile utasema nju yabo?
12 Wanze kuangaria muzuri. Ni muzuri kusali nju ya banduku na badada ba mingi ku mala moya, lakini ni muzuri tena kusali nju ya muntu moya-moya. Eske mu kutaniko yako muko muntu ule eko na malari ile aishake? Eske muko mutoto ule eko dekurajé nju barafiki yake ba ku masomo beko namusukuma kufanya mambo ya mubaya? Eske muko muzazi ule eko nakomarisha batoto ye moya na eko nafanya nguvu ya kubakomarisha kupatana na “mashauri ya Jeova na mambo ile eko natusopesha”? (Efe. 6:4) Kama unangaria muzuri, ile itafanya uendelee kujiweka pa fashi ya bengine na itakusukuma upende sana kusali nju yabo.b—Ro. 12:15.
13. Tunezi kufanya nini nju ya kusali nju ya bale atuyakunaka nabo?
13 Taya manjina ya bale uko nasali nju yabo. Tunezi kufanya vile ata nju ya bantu bale atuyakutanaka nabo. Kwa mufano, waza nju ya banduku na badada bale beko mu maprizon ya mu ma pays sa vile Creimée, Eritrée, Russie, na Singapoure. Utapata manjina ya bale beko mu maprizon ku jw.org.c Brian, mwangalizi wa muzunguko moya anasema ivi: “Minonaka asema kuanjika njina ya nduku ao dada ule eko mu prizon na kutaya ile njina kunanisaidiaka nimukumbuke na nimutaye mu sala yangu.”
14-15. Tunezi kulomba je mambo ile iko waji mu sala yetu?
14 Lomba mambo ile iko waji. Michael, ule turitaya tena, anasema ivi: “Saa minasomaka maabari ku jw.org ya banduku bale beko mu prizon, minapimaka kuwazia vile miripashwa kujishikia kama ni miye njo nirikuwa mu prizon. Minayuwa asema, kile kiripashwa kuniangaisha ni kuwaza vile bibi yangu atabakia, na ni nani njo atamwangaikia. Kuwaza vile kunanisaidia nipate mambo ya kuomba nju ya banduku bale beko mu maprizon benye bashakuoa.”—Ebr. 13:3, maelezo ya chini.
15 Kama tunawaza namna maisha ya kila shiku ya banduku bale beko mu maprizon inekalaka, tutapata mambo ya kuweka mu sala yetu. Kwa mufano, tunezi kusali nju bale beko nachunga banduku yetu mu maprizon bashibafanshie mubaya, na tunezi kusali nju bashefu bashikataze banduku yetu kumwabudu Jeova. (1 Ti. 2:1, 2) Tunezi kusali nju mufano ya banduku bale beko mu maprizon isaidie banduku ba mu makutaniko yabo ao tunezi kusali nju mufano ya bale banduku beko mu maprizon isaidie bale abana Batemwe baichike abari njema. (1 Pe. 2:12) Na tunezi tena kuwaza nju ya iyi mambo saa tunatafuta kusali nju ya banduku na badada bale beko napata magumu ingine. Saa tuko nangaria muzuri, tunataya manjina ya banduku yetu mu sala na tunalomba mambo ile iko waji, tutaonesha asema ‘mapendo yetu nju ya muntu na mwenzake . . . inayala sana.’—1 Te. 3:12.
UKUWE NA MAWAZO YA MUZURI SAA UKO NASALI
16. Namna kani tunezi kuwa na mawazo ya muzuri nju ya sala? (Matayo 6:8)
16 Saa vile turiona, kusali nju ya bengine kunezi kusaidia mambo iendeke muzuri. Lakini, tunapashwa kuwa na mawazo ya muzuri. Saa tuko nasali aina kusema tuko namuonesha Jeova mambo ile ashiyuwe ao tuko namupachia mashauri nju ya namna ya kwisha mambo fulani. Jeova anayuwa muzuri mambo ile batumishi bake beko nayo lazima ata mbele bo benyewe baiyuwe ao shiye bengine tuiyuwe. (Soma Matayo 6:8.) Sasa kama ni vile, nju ya nini tusali nju ya bengine? Kuongezea ku mambo ile tunatokea kuona mu iyi abari, ni nju tunapenda kuonesha asema tunabangaikia. Mapendo inatusukuma tusali nju ya bengine. Na Jeova anafurai sana saa anaona shiye batumishi bake tunapendana sa vile yeye anatupenda.
17-18. Leta mufano ile inaonesha vile Jeova anaonaka sala ile tunafanyaka nju ya banduku yetu.
17 Ata kama tunezi kuona asema ma sala yetu aisaidie mambo ikuwe muzuri, ma sala yetu inonesha asema tunapenda banduku na badada yetu na Jeova anaona ile. Tubebe iyi mufano: Wazia famiye moya iko na batoto bawiri; mutoto mwanaume na mutoto mwanamuke. Mutoto mwanaume analukula sana na eko mu kitanda, mutoto mwanamuke anamuriria baba yake ivi: “Papa saidiako mukubwa yangu nju ashikie bien eko malari sana.” Baba yake eko nafanya deja nguvu nju ya kusaidia mutoto yake ashikie muzuri, ule baba anapenda mutoto yake na eko namwangaikia muzuri. Ata vile, waza furaa ile ule baba atashikia saa anaona mutoto yake mwanamuke eko nangaikia sana mukubwa yake na eko namulomba baba yake amusaidie.
18 Njo vile na Jehova anapeda tufanye, anapenda twangaikiane na tusali nju ya bengine. Saa tunafanya vile, tunonesha asema atwangaikie tu mambo yetu shiye benyewe, lakini tunangaikia sana banduku na badada yetu na Jeova anaona vile. (2 Te. 1:3; Ebr. 6:10) Na sa vile turiona, sala inezi kusaidia mambo iendeke muzuri. Njo maana twendelee kufanya yetu yote nju ya kusali nju ya bengine.
MWIMBO 101 Tutumike kwa Umoja
a Turishanjé manjina ingine.
b Angaria ku jw.org video Takeshi Shimizu: Yehova Ni “Musikiaji wa Sala.”
c Nju ya kupata manjina ya banduku na badada yetu bale beko mu maprizon wende ku jw.org, anjika: “Mashahidi wa Yehova Wenye Kufungwa kwa Sababu ya Imani Yao—Kulingana na Eneo.”
d ESPLIKASION YA FOTO: Banduku na badada bale beko na magumu yabo beko nasali nju ya bengine.