Banduku bengine bawiri banaongezeka mu Collège central
LE 5 OCTOBRE, 2024, ku asamblé generale kurikuwa abari ya muzuri: Nduku Jody Jedele na nduku Jacob Rumph banaongezeka mu Collège central ya Batemwe de Jeova. Bote bawiri beko baaminifu na bashakumutumikia Jeova miaka ya mingi.
Jody Jedele na bibi yake Damaris
Nduku Jedele arizarikwa mu Missouri, mu Etats-Unis, na bazazi yake barikuwa Batemwe de Jeova. Famiye yake irikuwa nekala fashi ile murikuwa Batemwe kiloko tu. Njo maana, nduku Jedele arikutanaka na banduku ba mingi ba kutoka mafashi ya kwachana-achana bale baritembeleaka ile fashi nju ya kusaidia mu kaji ya maubiri. Mapendo ya bale banduku na vile barikuwa mu kimoya, njo irimusukuma na ye apende kufanya bya mingi mu kaji ya Jeova. Nduku Jedele aripata batem le 15 octobre 1983. Aripendaka sana kaji ya mauubiri, njo maana saa arishaka masomo ya sekondere arianzaka kaji ya bu painia mu septembre 1989.
Saa nduku Jedele arikuwaka mutoto, bazazi yake barianzaka kumupeleka, yeye na muloko yake mwanamuke, kutembelea Betel. Ile iribasaidia, yeye na muloko yake, bakuwe na amu ya kutumikia ku Betel. Na njo vile barifikiaka kwingiako. Nduku Jedele arifika ku Betel ya Wallkill mu septembre 1990. Arianzia mbele kutumikia mu Departema ya kusafisha na kisha aritumikaka mu Service medical.
Mu ile wakati, kurikuwa makutaniko ya Kiespanyole ile irikuwa karibu, irikuwa nendelea muzuri na irikuwa na lazima ya banduku. Njo maana nduku Jedele arianza kwingia mu kutaniko moya ya Kiespanyole na arianza kufunda ile luga. Kisha wakati kiloko, arikutana na dada Damaris, painia wa mu ile muzunguko. Kisha barioana, na dada Damaris ariingia na ye ku Betel.
Mu 2005, baritoka ku Betel nju ya kwenda kuchunga bazazi yabo. Mu ile wakati, baritumika sa vile bapainia ba kawaida. Nduku Jedele arisaidia kufundisha ku masomo ya bapainia na aritumika mu CLH (Comité de liaison hospitalier) ya mu fashi ile barianza kwikala. Na aritumika na mu Comité de construction régional.
Mu 2013, bariita tena nduku Jedele na bibi yake ku Betel nju batumike mu projet ya kuyenga Betel ya Warwick. Tangia pale, baritumikaku Patterson na ku Walkill. Nduku Jedelem aritumika mu LDC (Service local de développement-construction) na mu Service d’information hospitalier. Mu mars 2023, barimweka akuwe assistant mu Comité pour le service ya Collège central. Wakati nduku Jedele anakumbuka makaji ile arifanyaka nzamani, anasema ivi: “Saa banakupachia kaji ya sasa ya kufanya mu kaji ya Jeova, saa moya inezi kukwangaisha mu akiri, pale njo unapashwa kukumbuka kumutumainia Jeova, nju yeye njo atakusaidia kufanya bile byote anakulomba.”
Jacob Rumph na bibi yake Inga
Nduku Rumph arizarikwa mu Californie, mu Etats-Unis. Saa arikuwa mutoto, mama yake ashikwanzake kwenda ku ma renion na ashikwanzake kuubiri, lakini arianzaka kusumburia na nduku Rumph nju ya Bible. Tena, kila mwaka nduku Rumph arianza kutembelea kambo yake mwenye arikuwa Temwe de Jeova. Kambo yake arimusaidia apende kweri, na saa nduku Rumph arikuwa na miaka 13, arilomba baanze kumufundisha Bible. Nduku Rumph aripata batem le 27 septembre 1992, saa arikuwa angariki kiyana. Kintu kya kufuraisha ni kusema, mama yake arianza tena kwenda ku ma renion na kuubiri. Na baloko yake ya nduku Rumph bote bawiri na baba yake baripata batem.
Saa nduku Rumph arikuwa kiyana, ariona vile bapainia barikuwa na furaa. Njo maana, ile saa arisha masomo ya sekondere, arianza bu painia mu septembre 1995. Mu 2000, ariamia mu Equateur nju ya kutumikia kule. Kurikuwa lazima sana ya baubiri. Kule arikutana na dada Inga. Uyu dada arikuwa painia na kwabo kurikuwa ku Canada. Kisha mashiku, barioana. Kisha kuoana, baritumikia mu ville moya ivi ya mu Equateur, mule murikuwa ka nkikunji kaloko tu ka baubiri. Leo, kale ka nkikunji kashakuwa kutaniko ile iko nendelea muzuri.
Kisha wakati, nduku Rumph na bibi yake barifikia kuwa ba painia ba pekee, na kisha nduku Rumph arifikia kuwa mwangalizi. Mu 2011, baribaita ku masomo ya Galaad, mu classe ya 132. Kisha kupata diplome, baritumikia mu ma pays ya kwachana-achana. Barifuraia kutumika mu makaji ya kwachana-achana sa vile ku Betel, mu bu misionere, na mu bwangalizi. Nduku Rumph arifundishaka tena na ku masomo ya EER.
Nju ya malari ya Korona, nduku Rumph na bibi yake barirudia mu Etats-Unis. Baritumika ku Betel ya Wallkill, kule nduku Rumph aripata formation mu Département pour le service. Kisha baribarudisha tena ku Betel ya Equateur kule nduku Rumph aritumika mu Comité ya filiale. Mu 2023, baribatuma Warwick. Na mu janvier 2024, barimweka nduku Rumph kuwa assistant mu Comité pour le service ya Collège central. Saa anawaza nju ya fashi yote kule ashakutumikia, anasema ivi: “Kile kinafanyaka ufuraie kaji ile uko natumika, aina fashi kule uko natumikia, lakini ni bantu bale uko natumika nabo.”
Tunapenda sana kaji ya nguvu ya aba banduku, na ‘tunendelea kweshimia bantu ba ivi.’—Flp. 2:29.