ABARI YA KUFUNDA YA 47
MWIMBO 38 Atakupatia Nguvu
“Uko muntu wa maana sana”!
“Uko muntu wa maana sana.”—DA. 9:23.
MU KIFUPI
Kusaidia bale beko najishikia kuwa ba bule kukomprandre asema beko ba maana ku mancho ya Jeova.
1-2. Nini njo inezi kutusaidia tukuwe sire asema tuko ba maana sana kwa Jeova?
JEOVA anaonaka batumishi bake kuwa ba maana sana. Lakini batumishi bake bengine abajionake vile, pengine ni nju bantu baribatendeaka mubaya. Na weye unajionaka wa bule? Kama ni vile, nini njo itakusaidia ukuwe sire asema uko wa maana ku mancho ya Jeova?
2 Mu Bible muko maabari ile inaonesha asema Jeova anapendaka bantu batendee bengine muzuri. Kufunda ile maabari kutakusaidia sana. Yesu Mutoto yake ya Jeova, arieshimia bantu na aribatendea muzuri sana. Mambo ile Yesu arifanya inaonesha asema yeye na Baba yake banaonaka ata bantu bale banajionaka kuwa ba chini sana kuwa ba maana. (Yoh. 5:19; Ebr. 1:3) Mu iyi abari tutaona mambo mbiri: 1) Vile Yesu arisaidia bantu bajione kuwa ba maana na 2) namna tunezi kuwa sire asema tuko ba maana sana kwa Mungu.—Hag. 2:7.
NAMNA YESU ARISAIDIA BANTU BAYUWE ASEMA BEKO BA MAANA
3. Yesu aritendea je bantu ba mu Galilée bale barianza kumutafuta nju abasaidie?
3 Saa Yesu arianza kuubiri mu Galilée, bantu ba mingi barianza kuya kwake nju abafundishe na abaponeshe. Yesu ariona kama, “barikuwa bashakubatosha ngoji na akukukuwe wa kubangaikia sa bankodolo bale abana na wa kubachunga.” (Mt. 9:36.) Bakubwa yabo ya dini barianza kubaona kuwa ba bule, na abakuone asema ni kintu kya maana kubangaikia na barianza ata kubaita “bantu ba kulainiwa.” (Yoh. 7:47-49.) Lakini, Yesu yeye aribaona kuwa ba maana nju arianza kubeba wakati ya kubafundisha na kuponesha malari yabo. (Mt. 9:35) Tena nju ya kusaidia bantu ba mingi, Yesu ariformé ba mitume bake nju ya kuubiri na aribapachia uwezo ya kuponesha bantu.—Mt. 10:5-8.
4. Namna Yesu aritendea bale barionekana ba bule inatufundisha nini?
4 Yesu arieshimia bantu na aribatendea muzuri, ile inaonesha asema yeye na Baba yake banaona bantu kuwa ba maana ata kama bengine banabaona kuwa ba bule. Kama uko namutumikia Jeova lakini uko najiona wa bule, waza nju ya namna Yesu aritendea bantu bale baripenda abafundishe. Kufanya vile kutakusaidia uone asema uko wa maana kwa Jeova.
5. Ule mwanamuke Yesu arikutanaka naye mu Galilée arikuwa mu sitwasion kani?
5 Yesu arikuwa nafundisha bantu ba mingi, lakini arikuwa tena nafundisha na kusaidia muntu moya-moya. Kwa mufano, saa Yesu arikuwa naubiri mu Galilée arikutanaka na mwanamuke moya ule arifanya miaka 12 na malari ya kutoka damu. (Mk. 5:25) Kupatana na sheria, ule mwanamuke arikuwa wa buchafu nju ya ile malari, na kila muntu ule atamubamba na ye atakuwa wa buchafu. Njo maana, inawezekana ule mwanamuke arianza kwikala saa mingi pa ye moya. Tena ashikupashwe kumwabudu Jeova pamoya na bengine ao kwenda ku mafeti. (Law. 15:19, 25) Kusema tu bya kweri, ule mwanamuke ariteswa sana, arikuwa malari na arijiona kuwa wa bule.—Mk. 5:26.
6. Ule mwanamuke arikuwa na malari ya kutoka damu arifanya nini nju apone?
6 Mwanamuke wa malari ule arikuwa nateswa sana aripenda kwenda kumwona Yesu nju amuponeshe. Lakini ashikwende mala moya kule Yesu airikuwa. Nju ya nini? Pengine ule mwanamuke arianza kushikia aya nju ya malari ile arikuwa nayo. Ao pengine arianza kuongopa asema Yesu atamufokea nju anaingia mu nkikunji kya bantu na eko wa buchafu kupatana na sheria. Njo maana aribamba tu ku nguo ya inje ya Yesu na arikuwa sire asema kufanya vile kutamusaidia apone. (Mk. 5:27, 28) Jeova aribariki imani ya ule mwanamuke. Arifikia kupona. Yesu ariuliza ni nani njo arimubamba. Na ule mwanamuke arimonesha bile arifanya. Sasa Yesu arimutendea je?
7. Yesu arimutendea je ule mwanamuke? (Marko 5:34)
7 Yesu arieshimia ule mwanamuke na arimutendea muzuri. Yesu ariona asema ule mwanamuke “arianza kuongopa na kutetemeka.” (Mk. 5:33) Nju Yesu arijua vile, arisumburia naye muzuri na mambo ile arimwambia irimupachia nguvu. Yesu arimwita “mutoto yangu.” Ile misemo inaonesha asema Yesu arimweshimia, arimupenda na arimutendea muzuri. (Soma Marko 5:34.) Iyi njo fashi moya tu mu Bible mule Yesu anaita mwanamuke “mutoto yangu.” Pengine Yesu aritumikisha ile misemo nju ariona asema ule mwanamuke arikuwa eko ‘natetemeka.’ Unawaza ule mwanamuke arishikia je, saa ariona vile Yesu arikuwa nasumburia naye? Aripashwa kushikia furaa sana nju Yesu arimutendea muzuri na arimweshimia sana. Lakini, kama Yesu ashikusumburie naye vile, pengine aripashwa kurudia na ashakupona lakini wa mauzuni-uzuni. Yesu arimusaidia ule mwanamuke ayuwe asema Mungu anamwonaka kuwa mutoto yake wa maana sana na anamupenda.
8. Dada yetu moya wa mu Brésil arikuwa na magumu kani?
8 Leo kuko batumishi ba Jeova bengine bale beko na malari ile iko nabafanya bajishikie mubaya. Tubebe mufano ya dada Maria.a Yeye ni painia wa mu Brésil, arizarikaka pashipo mikulu na pashipo mukono ya gauche. Anasema ivi: “Ku masomo bantu barianza kunichokoza saa yote nju ya vile niko kilema. Barianza kunipanga manjina ya kunichokoza. Saa moya ata bantu ba mu famiye yangu barianzaka kunitendea mubaya.”
9. Nini njo irimusaidia dada Maria ayuwe asema eko wa maana kwa Jeova?
9 Nini njo irimusaidia dada Maria? Saa arifikia kuwa Temwe de Jeova, banduku na badada barimwankurajé na barimusaidia ajione vile Jeova eko namuona. Anasema ivi: “Banduku na badada ba mingi barinisaidia. Minamupikia Jeova merci na roo yote nju ya iyi famiye ya muzuri ya kiroo ile arinipachia.” Banduku na badada barimusaidia dada Maria akomprandre asema eko wa maana kwa Mungu.
10. Maria Magdalene arikuwa na magumu kani? (Angaria na mafoto.)
10 Ona vile Yesu arisaidia muntu mwingine. Ule muntu ni Maria Magdalene. Bademon ba 7 barikuwa basha kumwingia! (Lu. 8:2) Inawezekana bale bademon barianza kumusukuma kufanya bintu bile abina normal na ile irifanya bantu bakuwe mbari naye. Saa arikuwa na bale bademon arianza kuteswa sana, arijiona wa bule na kuwaza asema akuna muntu atamusaidia. Inawezekana Yesu arimutoshaka bale bademon na kwanzia pale Maria Magdalene arianza kumufwata Yesu. Yesu arifanya tena nini nju ya kumusaidia Maria Magdalene akomprandre asema eko wa maana kwa Mungu?
Yesu arifanya nini nju ya kumwonesha Maria Magdalene asema eko wa maana kwa Jeova? (Angaria mu paragrafe 10-11)
11. Namna kani Yesu arimusaidia Maria Magdalene akomprandre asema eko wa maana kwa Mungu? (Angaria na mafoto.)
11 Yesu arimupachia Maria Magdalene kaji ya maana sana ya kumusindikiza mu kaji ya maubiri.b Ile irimusaidia aendelee kumushikia Yesu saa eko nafundisha bengine. Tena saa Yesu arifufukaka, arimutokeaka Maria Magdalene. Arikuwa mu badisiple ba kwanza bale Yesu arisumburiaka nabo ile shiku. Yesu arimupachia ata kaji ya kwenda kwambia banafunzi bengine asema anafufuka. Mu ile mambo yote, Yesu arimusaidia Maria Magdalene aone asema eko wa maana sana kwa Jeova!—Yoh. 20:11-18.
12. Espliké nju ya nini mambo ile irimufikiaka dada Lidia irimufanya anze kujiona wa bule.
12 Saa vile pengine sitwasion ya Maria Magdalene irikuwa, bantu ba mingi leo banajishikiaka sa vile beko ba bule. Dada Lidia wa mu Espagne anasema kama ata mbele bamuzale, mama yake arianzaka kuwaza kutosha mimba yake. Anakumbuka asema ata pale arikuwaka mutoto sana, mama yake arianzaka kumwona wa bule na arianzaka kumusema mubaya. Dada Lidia anasema ivi: “Nju mama yangu ashikunioneshake mapendo, miripendaka bantu banipende na bapende kuwa barafiki yangu. Miriongopa asema akuna ata muntu moya ule atanipendaka nju mama yangu arianzaka kunionesha asema niko muntu mubaya.”
13. Nini irimusaidia dada Lidia akomprandre asema eko wa lazima ku mancho ya Jeova?
13 Saa dada Lidia arianza kufunda Bible, mambo irishanjé. Kusali, kusoma Bible, na misemo na matendo ya muzuri ya banduku na badada birimusaidia sana. Birimusaidia akomprandre asema eko wa maana sana ku mancho ya Jeova. Ye moya anasema ivi: “Mala mingi, bwana yangu ananiambiaka asema ananipendaka sana. Saa yote, ananikumbushaka bizuri byangu. Na barafiki yangu mu kutaniko bananiambiaka vile.” Na weye mu kutaniko yenu, unezi kufanya nini nju ya kusaidia muntu ule eko na lazima ya kukomprandre asema eko wa maana ku mancho ya Jeova?
NAMNA YA KUJIONA VILE JEOVA ANATUONAKA
14. 1 Samweli 16:7 inatusaidia je tujione vile Jeova anatuonaka? (Angaria na ankadré “Nju ya nini Jeova anaonaka bantu bake kuwa ba maana?”)
14 Kumbuka asema Jeova ashikuonake sa vile bantu ba mu iyi dunia banakuonaka. (Soma 1 Samweli 16:7.) Mu iyi dunia bantu banaonaka muntu kuwa wa maana nju ya namna anaonekana, makuta ile eko nayo ao masomo ile arifunda. (Isa. 55:8, 9) Lakini Jeova ye ashiangariake bile. Tafuta kujiona vile Jeova anakuonaka apana vile bantu ba mu iyi dunia banakuonaka. Unezi kusoma maabari ya mu Bible ya bantu bale Jeova ariona kuwa ba maana, ata kama saa moya bale bantu barianza kujiona kuwa ba chini; bantu sa vile Elie, Naomie na Anne. Unezi tena kwanjika mambo ile Jeova ashakukufanshiaka ile inaonesha asema anakupendaka na anakuonaka kuwa wa maana. Tena unezi kusoma maabari ile iko mu bitabu byetu ile inaonesha asema uko wa maana.c
15. Nju ya nini Jeova arimwona Daniel kuwa “muntu wa maana sana”? (Danieli 9:23)
15 Yuwa asema imani yako inakufanya ukuwe wa maana kwa Jeova. Daniel arijishikiaka ‘mwenye kuchoka sana’ na arikuwaka dekurajé. Iko sa ile wakati arikuwaka na miaka 90 na bya yulu. (Da. 9:20, 21) Jeova arifanya nini nju ya kumupachia nguvu? Arituma malaika Gabriel nju ya kumukumbusha asema arikuwa “muntu wa maana sana” na ma sala yake ariishikia. (Soma Danieli 9:23.) Nini njo irifanya Daniel akuwe wa maana kwa Jeova? Daniel arikuwa napenda kufanya mambo ya muzuri na arikuwa mwaminifu kwa Jeova. (Eze. 14:14) Jeova arianjikisha ile abari mu Bible nju itupachie nguvu. (Ro. 15:4) Jeova anashikiaka ma sala yako na anakuona kuwa wa maana nju unapenda kufanya mambo ya muzuri na nju uko mwaminifu kwake.—Mik. 6:8; Ebr. 6:10.
16. Nini njo inezi kukusaidia uyuwe asema Jeova ni Baba ule anakupendaka?
16 Yuwa asema Jeova ni Baba yako ule anakupendaka. Jeova anapenda kukusaidia, ashikalake pale nju ya kutafuta mankosa yako. (Zb. 130:3; Mt. 7:11; Lu. 12:6, 7) Kuwaza sana nju ya ile kurisaidia bantu ba mingi bale barianza kujiona kuwa ba bule. Tubebe mufano ya dada Eliana wa mu Espagne. Arianzaka kuona asema abamupende na arianza kujishikia kuwa wa bule nju bwana yake arianza kusumburia naye na makari sana. Ye moya anasema ivi: “Saa minajishikia kuwa wa bule, minapimaka kuwaza namna Jeova ananibeba mu mikono yake na ananionesha mapendo na ananichunga.” (Zb. 28:9) Dada Lauren, wa mu Afrique du Sud, anajikumbushaka iyi mambo: “Kama Jeova aritumikisha nkamba ya mapendo nju ya kunikokota kwake na ananifanya nibakie karibu naye iyi miaka yote, na arinipachia ata kaji ya kufundisha bantu bengine, niko sire asema ananionaka kuwa wa maana sana.”—Ho. 11:4.
17. Ni nini njo inezi kukusaidia ukuwe sire asema Jeova anakwichika kuwa muntu wake? (Zaburi 5:12) (Angaria na foto.)
17 Ukuwe sire asema Jeova anakwichika kuwa muntu wake. (Soma Zaburi 5:12.) David arionesha asema kuyuwa asema Jeova anaichika batumishi bake baminifu iko sa “kinvuri kya bujito” kile kiko natuchunga. Kuyuwa asema Jeova anatwichika na eko pale nju ya kutusaidia, kutatusaidia tushikuwe na madute na kwanza kuwaza asema atuna bantu bazuri. Sasa utayuwa je asema Jeova anakwichika? Sa vile turiona Jeova anatumikishaka Bible nju ya kutusaidia tuyuwe asema anatwichika. Tena anatumikishaka bazee, barafiki ba karibu na bantu bengine nju ya kutukumbusha asema tuko ba maana sana kwake. Utafanya nini saa bengine banakuonesha asema uko muntu muzuri?
Tutaacha kujiona kuwa ba bule kama tunakumbuka asema Jeova anatwichika kuwa bantu bake (Angaria mu paragrafe 17)
18. Nju ya nini tunapashwa kwichika saa bengine beko natwankurajé?
18 Saa bantu bale banakuyuwa na kukupenda banasema bizuri nju yako na banakwambia asema uko muntu muzuri, ushiwaze asema beko nakulanda. Kumbuka asema Jeova anezi kubatumikisha nju ya kukusaidia uyuwe asema anakupenda na anakuona kuwa wa maana. Dada Eliana, ule turitaya anasema ivi: “Polepole mirifikia kwanza kwichika mambo ya muzuri ile bengine beko naniambia. Irikuwa nguvu kwangu kwichika, lakini miriyuwa asema njo vile Jeova anapenda nifanye.” Bazee barimusaidia dada Eliana ayuwe asema Jeova anamupendaka. Leo, dada Eliana ni painia na mashiku ingine anasaidiaka kaji ku Betele.
19. Nju ya nini unezi kuwa sire asema uko wa maana ku mancho ya Mungu?
19 Yesu aritukumbusha asema tuko ba maana sana kwa Baba yetu wa ku mbingu. (Lu. 12:24) Njo maana tunapashwa kuwa sire asema Jeova anatuona kuwa ba maana, ile njo atupashwe kusabu ata shiku moya. Na twendelee kufanya yetu yote nju ya kusaidia bengine nabo bajione kuwa ba maana ku mancho ya Jeova!
MWIMBO 139 Wazia Uko mu Dunia Mupya
a Turishanjé manjina ingine.
b Inawezekana Maria Magdalene arikuwa mu banamuke bale barianzaka kumusindikiza Yesu. Bale banamuke baritumikisha bintu bile barikuwa nabyo nju ya kumwangaikia Yesu na ba mitume.—Mt. 27:55, 56; Lu. 8:1-3.
c Kwa mufano, soma shapitre 24 ya kitabu Approchez-vous de Jéhovah na usome mandiko na maabari ya mu Bible ile iko mu kitabu Maandiko ya Kutusaidia mu Maisha ya Kikristo pa titre “Mashaka.”