‘Mwendelee kuwa mu kimoya’
PAULO ariambiaka bakristo ba Efeso ivi: “Muvumiliane mu mapendo, na muko nafanya nguvu yenu yote nju ya kwendelea kuwa mu kimoya kupitia roo ya Mungu, mu nkamba ya amani ile inamiunganisha.”—Efe. 4:2, 3.
Ni roo ya Mungu njo inatusaidiaka kuwa mu kimoya. Lakini Paulo arisema kama tunapashwa kufanya nguvu yetu yote nju twendelee kuwa mu kimoya. Ni kusema kila mukristo eko na kile anapashwa kufanya nju ya “kwendelea kuwa mu kimoya kupitia roo ya Mungu.”
Tubebe mufano: Muntu anakupachia motoka ya sasa. Ni nani njo anapashwa kuiangaikia na kuichunga muzuri? Jibu iko waji. Autamushirikia ule arikupachia ile motoka kama inalabika nju aukuichunge muzuri.
Njo pamoya na shiye, kuwa mu kimoya ni kado ile Jeova aritupachia. Lakini, shiye bote tuko na kile tunapashwa kufanya nju twendelee kuwa mu kimoya. Kama atuna mu amani na nduku ao dada yetu, ni muzuri tujiulize ivi: ‘Eske niko nafanya kile minapashwa nju twendelee kuwa mu kimoya mu kutaniko?’
‘TUFANYE NGUVU YETU YOTE’ NJU YA KWENDELEA KUWA MU KIMOYA
Sa vile misemo ya Paulo inaonesha, saa moya aikalake teketeke kwendelea kuwa mu kimoya na banduku na badada surtout kama nduku ao dada aritukosea. Eske nju ya kwendelea kuwa mu kimoya inalomba tu kwita ule muntu aritukosea nju ya kumuonesha bibaya bile aritufanshia? Apana, ailombe paka tufanye vile. Ujiulize ivi: ‘Kama minaendelea kufwatiria iyi mambo, italeta amani ao njo itafanya mambo ialabike sana?’ Saa moya kintu kya muzuri kya kufanya ni kurumia ule muntu na kusabu ile mambo.—Mez. 19:11; Mk. 11:25.
Ujiulize ivi: ‘Kama minaendelea kufwatiria iyi mambo, italeta amani ao njo itafanya mambo ialabike sana?’
Sa vile Paulo arianjika, twendelee ‘kuvumiliana mu mapendo.’ (Efe. 4:2) Kitabu kimoya kinasema kama ile misemo inezi kuwa na maana ya “kubaichika vile beko.” Ni kusema, tunaichika asema banduku yetu nabo banafanyaka mankosa sa shiye. Kusema tu bya kweri, shiye bote tuko najikaza kuvala “bumuntu bwa sasa.” (Efe. 4:23, 24) Na akuna ata muntu moya ule ashakuwa mukamilifu. (Ro. 3:23) Kama tunaweka ile mu akiri itakuwa teketeke kwetu kuvumiliana, kurumiana, na “kwendelea kuwa mu kimoya kupitia roo ya Mungu.”
Tutakuwa mu ‘nkamba ya amani ile inatuunganisha’ mu kutaniko kama tunarumia banduku yetu na kusabu mankosa ile baritufanshia. Maneno ya mu kigreke ile irileta misemo “nkamba ya amani” mu Waefeso 4:3 inezi kumanisha tumankamba twa tuloko-tuloko twa nguvu tule tunaunganishaka mifupa. Tule tumankamba tunekalaka nguvu sana nju tunaunganishaka mufupa moya na ingine. Njo pamoya na amani na mapendo; biko sa tule tumankamba, binatusaidiaka tukuwe karibu na banduku yetu ata kama saa moya atupatane.
Saa muntu anakukosea ao anakufanshia kintu kile aukupende, pima kumukomprandre kuriko kutafuta-tafuta mankosa yake. (Kol. 3:12) Nju shiye bote tunafanyaka mankosa, na weye saa moya unakoseanaka. Kukumbuka ile kutakusaidia kufanya yako yote nju ya “kwendelea kuwa mu kimoya kupitia roo ya Mungu.”