Abari ya kusaidia banamuke bale banatendeaka mubaya
“ MU DUNIA mujima banatendeaka banamuke mubaya. Na weye uko mu bale banamuke? Ona nju ya nini Mungu anangaikiaka banamuke na anapendaka babatendee muzuri, na kile atafanshia bale beko nabatendea mubaya.”
Ile njo maneno ya kwanza ya mu abari “La sécurité des femmes: Ce qu’en dit la Bible.” Ile abari iko ku jw.org. Ku mwisho ya ile abari kuko lien ile itakusaidia kutelesharjé dokima ile unezi ku imprimé na kukunja nju ifanane trakte ya ma paje 4. Dada Stacy wa mu Étas-Unis anasema ivi: “Niri imprimé ma kopi ya ile abari, na miye na dada mwingine turiipeleka fashi kule banamuke bale banatendeaka mubaya banakimbiriaka.”
Mwanamuke moya ule anatumikaka ku ile nyumba ariuliza kama anezi kupata ma kopi ingine ya ile abari nju ya kupachia bale banekalaka mu ile nyumba. Ile irifanya bale badada bawiri bakabule ma kopi ingine 40 ya ile matrakte, na makarte 30 ya jw.org. Kisha, saa barirudia tena, ule anashimamiaka ile nyumba aripenda batemwe baoneshe banamuke bale banekalaka mu ile nyumba namna banafundishaka bantu Bible.
Saa dada Stacy na badada bengine bawiri baritembelea nyumba ingine kule banamuke bale banatendeaka mubaya banakimbiriaka, baripata ma resultat ya muzuri nju kisha kupeleka ma kopi 5 ya ile trakte, baribalomba tena ma kopi ingine ya mingi. Mwanamuke moya ule anatumikaka ku ile nyumba arisema ivi: “Iyi trakte itasaidia banamuke bale banekalaka uku.” Na ariongeza tena ivi: “Tuko na lazima sana nayo.” Saa bale badada barirudia tena kule, banamuke ba mingi baripenda kuona vile batemwe banafundishanaka Bible, na banamuke bawiri barisema kama baripenda kwenda ku renion ya juma ile irifwata.
Dada Stacy anasema ivi: “Turishangaa sana kuona vile bantu baripenda sana kusoma iyi abari. Ku imprimé na kukabula ile trakte ni namna ya muzuri ya kupeleka abari ya ufalme ku banamuke bale bantu banatendeaka mubaya. Turifurai sana kuona namna bale banamuke baripokea ile abari, na tuko na furaa sana kuona vile Jeova eko natusaidia saa tuko nendelea kuubiri abari njema ku bale banamuke.”