Maulizo ya bale banasomaka bitabu byetu
Mu wakati ya ku mbele ile iko karibu, ni “wazo” kani ile Jeova ataweka mu ma roo ya maguvernema?
Ufunuo 17:16, 17 inasema ivi nju ya mwanzo ya mateso ya nguvu sana (ao taabu kubwa) : “Masengo 10 ile uriona na ule nyama wa pori, batamuchukia ule ndumba na batamwacha mikono waji na bunji, na batakurya nyama yake na batamulungusha ye wote. Nju Jeova njo ariweka kile kintu mu akiri yabo nju batimize wazo yake, ndiyo, ile wazo yabo moya ya kupachia ule nyama wa pori maguvernema yabo.” Nzamani mu bitabu byetu turianzaka kusema kama “wazo” ile Jeova ataweka mu ma roo ya maguvernema ni ya kwalabisha makanisa ao ma religion yote ya bongo.
Lakini, turiona kama ni muzuri kutengeneza pale. “Wazo” ile Jeova ataweka mu ma roo ya maguvernema ni nju bapachie “ule nyama wa pori maguvernema yabo.” Nju ya kuyuwa vile ile mambo itafanshika, acha tutafute majibu ya iyi maulizo.
Ni ba nani njo beko mu iyi profesi? “Ndumba” ule banaita tena “Babilone munene” njo makanisa yote ya bongo. Ule “nyama wa pori wa rangi ya rouge ya kwangala” njo Organisation de Nations unies. Irianza kutumika tangu 1919 nju ya kuleta amani mu dunia, na irikuwa na njina Société des Nations. (Ufu. 17:3-5) “Masengo 10” ni maguvernema ile iko natumika pamoya na ule nyama wa pori.
Ni nini inaunganisha ule ndumba pamoya na ule nyama wa pori wa rangi ya rouge ya kwangala? Ule ndumba “ashakwikala yulu” ya ule nyama wa pori, ni kusema eko namuunga mukono na eko natafuta ule nyama wa pori afwate bile ye anapenda.
Ni kintu kani kitamufikia ule ndumba? Ule nyama wa pori, pamoya na ile masengo 10, “batamuchukia sana ule ndumba.” Njo maana batamunyanganya bintu byake byote na kuonesha bubaya bwake waji-waji. Batamwalabisha, njo vile Jeova arisemaka nju yake. (Ufu. 17:1; 18:8) Ile njo itakuwa mwisho ya makanisa ya bongo. Lakini mbele ile mambo ifanshike, Jeova atasukuma maguvernema ifanye kintu kimoya kile aiyafanyaka ata shiku moya.
Jeova atasukuma maguvernema ifanye nini? Jeova ataweka “wazo yake” mu ma roo ya ile masengo 10, ile wazo ni “kumupachia ule nyama wa pori wa rangi ya rouge ya kwangala nguvu yabo na mamlaka yabo.” Ule nyama wa pori ni Nations Unies. (Ufu. 17:13) Eske maguvernema itadesidé tu yo yenyewe kumupachia ule nyama wa pori nguvu yabo na mamlaka yabo? Apana, aina vile! Profesi inaonesha asema Mungu ye mwenyewe njo atabasukuma kufanya vile. (Mez. 21:1; komparé na Isaya 44:28.) Eske maguvernema itakuwa napachia polepole ule nyama wa pori nguvu na mamlaka yabo? Apana, abitakuwa vile! Ile mambo itafanshika mbio-mbio, na itakuwa ya kushitusha. Nyama wa pori ule atakuwa sasa na nguvu ya mingi sana atalabisha sasa bya lote makanisa yote ya bongo.
Tuko nachunga sasa nini ifanshike? Atutachunga ma information ile inaonesha asema maguvernema iko naunga mukono polepole Nations Unies. Kile tunezi kuchunga kifanshike ni iki: Jeova atafanya maguvernema yote ipachie Nations Unies nguvu yabo, na ile itafanshika mala moya na itakuwa ya kushitusha. Saa ile mambo itafanshika, tutayuwa asema mateso ya nguvu sana inatafuta kwanza. Saa tuko nachunga ile mambo ifanshike, “twendelee kubakia mancho na tuchunge akiri yetu” nju mambo ya kushitusha iko karibu kufika!—1 Te. 5:6