MAWAZO YA MU BIBLE
Tumikisha “kado ya kiroo” ile uko nayo
Kupitisha wakati pamoya na banduku na badada yetu kunatupachiaka nguvu sana. Lakini nju ile wakati itwankurajé tena sana, kuko kintu kingine kile tunapashwa kufanya. Bible inaita ile kintu “kado ya kiroo.” Njo kusema uwezo ya kwankurajé bengine ile tuko nayo. (Ro. 1:11, 12) Namna kani tunezi kutumikisha muzuri sana ile kado?
Tumikisha misemo ya kwankurajé. Kwa mufano, saa uko naleta jibu ku renion ushiseme mawazo yako ao kusema mambo ya mingi nju yako. Lakini, sema nju ya bile urifunda nju ya Jeova, bile urifunda mu Bible, na nju ya bile unafunda kupitia imani ya bakristo bengine baminifu. Saa uko nasumburia na nduku ao dada yako, sema mambo ile itamwankurajé.
Ankurajé bengine kupitia matendo yako. Kwa mufano, kuko bale banadesidé kwendelea kufanya utumishi ya wakati yote ata kama beko na ma probleme yabo. Bengine banafanyaka yabo yote nju ya kufika ku ma renion ya mu kachi-kachi ya juma ata kama biko nguvu kwabo nju ya kaji ile banatumikaka ao nju ya malari ile beko nayo.
Eske misemo na matendo yako binaankurajaka banduku na badada? Eske na weye unaonaka bile banduku na badada yako banasemaka ao kufanya nju ya kukwankurajé?