ABARI YA KUFUNDA YA 48
MWIMBO 129 Tutaendelea Kuvumilia
Kitabu kya Yobu kinezi kukusaidia saa uko mu magumu
“Kusema tu bya kweri, Mungu ashiwezi kufanya mambo ya mubaya.”—YOBU 34:12.
MU KIFUPI
Kitabu kya Yobu kitatufundisha nju ya nini Mungu anacha mateso na vile tunezi kuivumilia.
1-2. Nju ya nini ni muzuri tusome kitabu kya Yobu?
ESKE panakawia tangu usome kitabu kya Yobu? Ata kama barikianjika kushakupita miaka 3 500, bantu ba mingi banasemaka asema kitabu kya Yobu barianjikaka muzuri sana. Bantu ba mingi banatapaka ule arianjika kile kitabu nju aritumikisha misemo ya teketeke na ya muzuri sana. Moïse njo arianjikaka kile kitabu, na Jeova njo arimuongozaka anjike kile kitabu.—2 Ti. 3:16.
2 Kitabu kya Yobu ni kitabu kya maana sana mu Bible. Nju ya nini? Nju kinatusaidia kukomprandre asema bamalaika na bantu banapashwa kumutumikia Jeova nju banamupenda na nju banapenda njina yake. Tena, kinatusaidia tuyuwe vile Jeova anekalaka: Anekalaka na mapendo, ekima, aki na nguvu. Kwa mufano, mu kitabu kya Yobu banamwita Jeova “Muweza-yote” mala 31. Kama tunaweka pamoya bitabu byote bya mu Bible na tunabalula mala ile banamwita Jeova “Muweza-yote,” tutavumbula asema ni mu kitabu kya Yobu tu njo banamwita Jeova kuwa Mungu Muweza-yote mala mingi. Kitabu kya Yobu kinajibu maulizo ile tunajiulizaka mu maisha, na kinaleta jibu ku iyi ulizo ile inangaishaka bantu ba mingi: Nju ya nini Mungu anacha bantu bateswe?
3. Kufunda kitabu kya Yobu kutatusaidia je?
3 Sa vile kupanda ku murima kunasaidiaka muntu aone muzuri bintu bile binamujunguluka, kusoma kitabu kya Yobu kutatusaidia kukomprandre muzuri mawazo ya Jeova nju ya mateso yetu. Acha tuone sasa vile pengine abari ya Yobu irisaidia batoto ba Israel na vile inezi kutusaidia leo. Tena tutaona namna tunezi kutumikisha kitabu kya Yobu nju ya kusaidia bengine.
MUNGU ARIACHA YOBU ATESWE
4. Yobu arikuwaka ashakwachana je na batoto ba Israel bale barikuwaka mu Egypte?
4 Saa batoto ba Israel barikuwaka batumwa mu Egypte, Yobu arianzaka kuishi mu Ouz. Inawezekana ile mukini irikuwaka karibu na Arabie. Saa batoto ba Israel bengine mu Egypte barianzaka kwabudu masanamu, Yobu yeye arianzaka tu kumutumikia Jeova na roo moya. (Yos. 24:14; Eze. 20:8) Jeova arisemaka ivi nju ya Yobu: “Pa dunia akuna muntu sa yeye.”a (Yob 1:8) Yobu arikuwaka na mari ya mingi sana, na bantu ba fashi ile arianzaka kuishi barianzaka kumweshimia sana. (Yob 1:3) Shetani arishirikaka sana kuona vile Yobu, muntu ule bantu ba mingi bariyuwa na kweshimia, arikuwaka namutumikia Jeova na roo moya!
5. Nju ya nini Jeova arimwachaka Yobu ateswe? (Yob. 1:20-22; 2:9, 10)
5 Shetani arisemaka kama Yobu atacha kumutumikia Jeova kama tu anapata mateso. (Yob. 1:7-11; 2:2-5) Jeova arimupendaka sana Yobu, lakini arimwachaka Shetani aoneshe kama bile arisemaka nju ya Yobu ni bya kweri ao ni bya bongo. (Yob. 1:12-19; 2:6-8) Shetani arimuwia Yobu bivuko byake byote, arimuwia batoto yake bote ba 10, na arimufanya alukule malari ya nguvu sana ile irimubamba maungu mujima. Ata kama Shetani arimuteswa sana, Yobu yeye ariendeleaka tu kumutumikia Jeova na roo moya. (Soma Yobu 1:20-22; 2:9, 10.) Kisha wakati, Jeova arimurudishia tena Yobu santé ya muzuri, mari yake, arifanya tena bantu baanze kumweshimia sana, na arimupachia batoto bengine ba 10. Jeova arirefusha ata maisha ya Yobu. Yobu ariishi miaka 140 na arifikia kuona bankana na bankanununa. (Yob. 42:10-13, 16) Iyi abari ya Yobu irisadiaka je bantu ba nzamani, na inezi kutusaidia je na shiye leo?
6. Abari ya Yobu iripashwaka kusaidia je batoto ba Israel? (Angaria na foto.)
6 Abari ya Yobu iripashwa kusaidia je batoto ba Israel? Maisha ya batoto ba Israel aikukuwake teketeke mu Egypte. Josué na Caleb baripitisha buyana bwabo bote mu butumwa. Kisha, nju ya nkosa ya bantu bengine, barijungulukaka miaka 40 mu dezer. Kama batoto ba Israel bariyuwaka magumu ile Yobu aripataka na namna Mungu arimusaidiaka, kusema tu bya kweri, ile iribasaidiaka bo na batoto yabo bayuwe asema ni Shetani njo analetaka mateso, aina Mungu. Ile abari iripashwaka tena kubasaidia bakomprandre muzuri nju ya nini Mungu anachaka mateso, na bakomprandre asema Mungu anafuraiaka kama bantu beko baminifu kwake na beko namutumikia na roo moya.
Ku mwisho, kisha batoto ba Israel kutumika miaka mingi mu butumwa mu Egypte, barifikiaka kuyuwa mambo ile irimufikiaka Yobu (Angaria paragrafe 6)
7-8. Kitabu kya Yobu kinezi kusaidia je bale beko nateswa? Leta mufano.
7 Abari ya Yobu inezi kutusaidia je na shiye leo? Bantu ba mingi leo bashakupotesha kitumaini kwa Mungu nju abakomprandre nju ya nini mambo ya mubaya iko nafikia bantu bazuri. Na ile inauzunisha sana. Tuone mambo ile irimufikiaka dada Hazelb wa mu Rwanda. Saa arikuwaka mutoto, arianzaka kumwamini Mungu. Lakini mambo ya mubaya irimufikiaka mu maisha. Mama yake na baba yake bariachana. Mama yake aripata bwana mwingine, na ule bwana arianza kumuteswa dada Hazel. Kisha mashiku, mwanaume moya arimuviolé. Dada Hazel arienda ku kanisa yake na kuwaza asema atashikiako mambo ile itamupachia nguvu. Lakini ashikuipate. Kisha, dada Hazel arianjika mambo ile aripenda kumwambia Mungu. Arianjika ivi: “Mungu, mirianza kukuomba, mirianza kufanya nguvu yangu yote nju ya kufanya bizuri, lakini weye urianza kunirudishia tu paka bibaya. Sasa minakwacha, na mitafanya byote bile bitanifuraisha.” Sa tu vile dada Hazel, bantu ba mingi leo banamini mambo ya bongo ile baribaambiaka nju ya Mungu. Banamini asema Mungu njo analeteaka bantu mateso! Tunabashikiriaka buluma bale bantu, na tunapendaka kubasaidia bayuwe kweri nju ya Mungu.
8 Kupitia mambo ile tunafunda mu kitabu kya Yobu, shiye tunayuwa asema aina Mungu njo analeteaka bantu mateso, lakini ni Shetani! Tena, tunayuwa asema kama bantu beko nateswa aina nju ya mambo ya mubaya ile barifanyaka nzamani. Sa vile Mandiko inaonesha, “wakati na mambo ile atuwazie” inafikiaka bantu bote. (Muh. 9:11; Yob. 4:1, 8) Tena tunafunda asema kama tunavumilia magumu na tunaendelea kuwa baminifu, tunamupachia Jeova okazion ya kuonesha asema Shetani ni wa bongo. (Yob. 2:3; Mez. 27:11) Tunamupikia Jeova merci sana nju aritumikisha Bible nju ya kutusaidia tuyuwe kile kinafanyaka shiye na bantu bengine tuteswe. Kisha, dada Hazel arifikia kufunda Bible na Batemwe de Jeova. Arifikia kuvumbula asema aina Mungu njo anatuleteaka mateso. Arisema ivi: “Mirisali tena kwa Mungu na mirimufunguria roo yangu yote. Saa mirimwambiaka asema minamwacha, aina asema miripendaka kwacha kumutumikia. Mirisemaka vile nju shikumuyuwake muzuri. Leo minakomprandre asema Jeova ananipendaka, na niko na furaa sana.” Tunamupikia Jeova merci sana nju anatusaidia tuyuwe nju ya nini anachaka bantu bateswe! Tuone sasa namna abari ya Yobu inezi kutusaidia saa tuko mu mateso.
ABARI YA YOBU INATUSAIDIA KUVUMILIA
9. Espliké vile mateso ya Yobu irikuwa (Yakobo 5:11)
9 Pima kuwaza mateso ile Yobu arikuwa nayo: Ashakwikala chini pa maivu. Eko na bivimbo maungu mujima na biko namuuma sana. Ngoji yake ishakwalabika sana, na ashakukonda sana. Yobu ashina na nguvu, eko naripalula na kipande kya nsani ya bulongo. Na mala mingi, eko naritompolea nju ya maumivu yake. Saa Yobu arikuwa mu mateso ashikwanze tu kuchunga lufu, lakini ariendelea kubakia mwaminifu kwa Jeova na arimutumainia. (Soma Yakobo 5:11.) Ni nini njo irimusaidiaka Yobu kuvumilia?
10. Ni nini njo inaonesha asema Yobu arikuwa na burafiki bwa karibu sana na Jeova? Espliké
10 Yobu arikuwa na burafiki bwa karibu sana na Jeova, njo maana arimwambia mambo yote ile arikuwa nayo ku roo. (Yob. 10:1, 2; 16:20) Kwa mufano, mu shapitre 3, Yobu anaonesha maumivu ile arikuwaka nayo ku roo nju ya mambo ile irimupata. Yobu ariwaza asema ni Jeova njo arimuletea ile mambo yote. Kisha, barafiki yake ba 3 barimwambia mala na mala asema Mungu njo arikuwa namupachia punition nju ya manzambi yake. Lakini Yobu ariendelea kusema kama ashina na nkosa na eko mwaminifu kwa Jeova. Saa moya kuko mambo ile Yobu arianza kusema ile irionesha kama arianza kuriona asema eko jiste kumupita Mungu. (Yob. 10:1-3; 32:1, 2; 35:1, 2) Njo pale, ata ye moya arifikia kukomprandre asema saa moya arianzaka kusema “mambo yashipo mu njia nju aripendaka kuonesha asema ashina na nkosa.” (Yob. 6:3, 26) Na mu shapitre 31, Yobu anapenda Mungu amujibu, anaonesha asema ashikufanye kintu kibaya nju apate ile mateso. (Yob. 31:35) Lakini Yobu ashikupashwe paka kumukankamisha Mungu amwambie nju ya nini arianza kuteswa.
11. Jeova arifanya je nju ya kumujibu Yobu?
11 Tunakomprandre asema, kama Yobu arianza kusumburia vile na Jeova, ni nju arikuwa na burafiki bwa nguvu sana pamoya naye, na arikuwa sire asema Jeova ataona asema ashina na nkosa na atamufanshia mambo ya muzuri. Jeova arifanya kukuwe mpepo ya nguvu na arianza kumujibu Yobu. Lakini, Jeova ashikumuoneshe Yobu nju ya nini arikuwa eko nateswa, na ashikumupachie Yobu punition nju arisema kama ashikufanye kintu kibaya. Lakini sa baba wa roo ya muzuri, Jeova arimufundisha Yobu namna ya muzuri ya kuwaza. Na ile irikuwa njia ya muzuri ya kumusaidia Yobu. Ku mwisho, Yobu arikomprandre asema ashikuyuwe mambo mingi, na arilomba buluma nju ya misemo yashipo mu njia ile arisema. (Yob. 31:6; 40:4, 5; 42:1-6) Pengine iyi abari irisaidia je bantu ba nzamani, na inezi kutusaidia je na shiye leo?
12. Pengine abari ya Yobu irisaidia je batoto ba Israel?
12 Pengine abari ya Yobu irisaidia je batoto ba Israel? Pengine mambo ile irimufikia Yobu irifundisha batoto ba Israel mambo mingi. Tubebe mufano ya Moïse. Aikukuwe teketeke kwake kuongoza batoto ba Israel, nju mala mingi abakukuwe beko namushikia Jeova na barianza kufanya mambo ile irianza kufanya Moïse ajishikie mubaya. Saa mambo irikuwa nguvu, batoto ba Israel barianza kutompola ku mbele ya Jeova, lakini Moïse yeye ashikukuwe vile. Saa mambo irikuwa nguvu, arianza kusali kwa Jeova na kumwambia bile arikuwa nabyo ku roo. (Kut. 16:6-8; Hes. 11:10-14; 14:1-4, 11; 16:41, 49; 17:5) Pengine abari ya Yobu irimusaidia sana Moïse saa Jeova arimupachia punition. Kwa mufano, saa batoto ba Israel barikuwa fashi ile banaita Kadesh, pengine mu mwaka yabo ya 40 ya kujunguluka mu dezer, “pashipo kuwaza” Moïse arisema mambo ya mubaya na ashikufanye bantu bamupachie Jeova utukufu. (Zb. 106:32, 33) Na ni nju ya ile njo Jeova arimwambia Moïse asema ashitengia mu inchi ya malako. (Kum. 32:50-52) Ni kweri Moïse aripashwa kushikia mubaya saa arishikia vile, lakini arijishusha na kwichika bile Jeova arimuonesha. Pengine abari ya Yobu irisaidia na batoto ba Baisrael bale barizarika kisha wakati ya Moïse. Kuwaza sana nju ya abari ya Yobu, kuripashwa kusaidia batoto ba Israel baminifu ba nzamani, bayuwe namna ya kumwambia Jeova bile beko nabyo ku roo, na iripashwa kubasaidia bashijione sa bantu ba aki sana kumupita Jeova. Tena iyi abari ya Yobu iripashwa kubasaidia bajishushe na kwichika bile Jeova eko nabaambia.
13. Kitabu kya Yobu kinezi kutusaidia je? (Waebrania 10:36)
13 Abari ya Yobu inezi kutusaidia na shiye je? Tuko naishi mu wakati ya nguvu, njo maana tuko na lazima ya nguvu nju twendelee kuvumilia na kumutumikia Jeova. (Soma Waebrania 10:36.) Kwa mufano, pengine tuko malari sana ao tuko na mangaiko ya mingi, ao tena tuko na magumu mu famiye. Pengine turifisha ao tuko na magumu ingine. Saa moya, matendo na misemo ya bengine inezi kufanya ikuwe nguvu kwetu kuvumilia. (Mez. 12:18) Lakini, kitabu kya Yobu kinatufundisha asema tunezi kumwambia Jeova mambo yote ile tuko nayo ku roo, na kuwa sire asema atatushikia. (1 Yo. 5:14) Jeova ashitatushirikia kama tunamwambia vile tuko najishikia, ata kama saa moya tunasema “mambo yashipo mu njia.” Lakini, Jeova atatupachia nguvu na ekima ile tuko nayo lazima nju tuvumilie. (2 Ny. 16:9; Yak. 1:5) Na kama ni lazima, Jeova anezi kutusaidia tukuwe na mawazo ya muzuri sa vile arimusaidiaka Yobu. Jeova anezi kutupachia mashauri kupitia Bible, bitabu byetu, muzee wa kutaniko ao rafiki mwingine. Mufano ya Yobu inatufundisha asema, saa Jeova eko natupachia disipline, tunapashwa kwichika. (Ebr. 12:5-7) Mambo irikuwa muzuri kwa Yobu nju arimushikia Jeova. Na shiye kama tunajishusha na tunechika mashauri, mambo itakuwa muzuri kwetu. (2 Ko. 13:11) Iyi ni mambo ya lazima sana ile kitabu kya Yobu kinatufundisha! Acha sasa tuone namna tunezi kutumikisha kitabu kya Yobu nju ya kusaidia bengine.
TUMIKISHA KITABU KYA YOBU NJU YA KUSAIDIA BENGINE
14. Ni njia kani tunezi kutumikisha mu maubiri nju ya kusaidia bantu bakomprandre kile kinafanyaka bantu bazuri bateswe?
14 Eske ushakukutanaka na muntu mu maubiri ule anakuuliza nju ya nini kuko mateso? Urimujibwaka je? Pengine urimwambiaka mambo ile Bible inasema, ile irifanshikaka mu jardin ya Eden. Pengine urianzaka na kumwambia asema Shetani, ule malaika mubaya, njo arilandaka bazazi yetu ba kwanza, na ile irifanya bamugeukie Mungu. (Mwa. 3:1-6) Tena, pengine urimwambiaka asema nju Adam na Eve abakumushikie Mungu, bantu barianza sasa kuteswa na kufwa. (Ro. 5:12) Kisha, pengine urimwambiaka asema Mungu ashakwacha wakati ya kwenea ipite nju kila muntu ajionee asema Shetani arisemaka bongo. Na tena, pengine urimwambiaka asema Mungu eko natumikisha iyi wakati nju ya kusaidia bantu bayuwe asema atatosha mateso na atabapachia maisha ya furaa milele. (Ufu. 21:3, 4) Ile ni namna ya muzuri ya kujibu, na inezi kusaidia bantu ba mingi bakomprandre nju ya nini bantu bazuri banateswaka.
15. Tunezi kutumikisha je kitabu kya Yobu nju ya kusaidia muntu ule anauliza nju ya nini kuko mateso? (Angaria na mafoto.)
15 Namna ingine ya kuespliké muntu akomprandre nju ya nini mateso ikwako ni kumuonesha abari ya Yobu. Unezi mbele kumupikia ule muntu merci nju anauliza ulizo ya maana. Kisha, unezi kumwambia asema ata Yobu mutumishi mwaminifu, saa aripataka magumu, arijiulizaka vile. Arianzaka ata kuwaza asema ni Mungu njo eko namuletea ile mateso. (Yob. 7:17-21) Ule muntu uko nasumburia naye anezi kushangaa kuyuwa asema tangu nzamani bantu banapendaka kuyuwa nju ya nini kuko mateso. Kisha, unezi kumuonesha asema, vile kitabu kya Yobu kinaonesha, aina Mungu njo arimuleteaka Yobu mateso, lakini ni Shetani njo ariiletaka. Shetani arisemaka asema, kama bantu beko namutumikia Mungu, ni nju ya bizuri bile eko nabapachia. Lakini kama banateswa batacha kumutumikia. Unezi kuongeza ivi: Ata kama aina Jeova njo arimuleteaka Yobu mateso, arimwachaka Yobu ateswe. Ile inaonesha asema Mungu eko sire na batumishi bake baminifu. Eko sire asema bataonesha kama Shetani ni wa bongo. Ku mwisho, unezi kumuonesha asema Yobu aribakiaka mwaminifu ata kama ariteswa, na Mungu arimubariki sana. Njo maana, tunezi kusaidia bengine na kubaonesha asema aina Jeova njo eko natuletea mateso.
Unezi kutumikisha je kitabu kya Yobu nju ya kusaidia bengine bayuwe asema Jeova ashileteake bantu mateso? (Angaria paragrafe 15)
16. Leta mufano ile inaonesha vile kitabu kya Yobu kirisaidia muntu ule arianza kuteswa.
16 Ona vile kufunda kitabu kya Yobu kurisaidia mwanaume moya. Ule mwanaume njina yake ni Mario. Shiku moya mu 2021, dada moya arikuwa eko naubiri ku telefone. Saa ariita mala ya kwanza arisumburia na Mario. Arimusomea versé ile inaonesha asema Mungu anashikiaka maombi yetu na anatulaka maisha ya muzuri uku ku mbele. Kisha, saa ule dada arimuuliza mawazo yake, Mario arijibu asema arikuwa nanjikia famiye yake mukanda nju ya kubaonesha asema anabapendaka sana, na kisha aritafuta kuriuwa. Mario arisema ivi: “Nishakumwamini Mungu, lakini minaona sa ashiniangaikiake.” Saa ule dada ariita tena, barisumburia nju ya abari ya Yobu na mateso ile aripataka. Mario aridesidé kusoma kitabu kyote kya Yobu. Ule dada arimutumia lien ile irimupeleka mu Biblia Tafsiri ya Ulimwengu Mupya. Mambo iriendelea je? Mario ariichika kufunda Bible na aripenda kufunda mambo ya mingi sana nju ya Mungu, nju ariyuwa asema Mungu eko na mapendo na anamwangaikiaka.
17. Nju ya nini tuko na furaa kuona vile Jeova arianjikisha abari ya Yobu mu Bible? (Yobu 34:12)
17 Sauti ya Mungu iko na nguvu ya kusaidia bantu, ata bale beko mu mateso. (Ebr. 4:12) Tuko na furaa sana nju Jeova arianjikisha abari ya Yobu mu Bible na tunezi kuisoma leo! (Yob. 19:23, 24) Kitabu kya Yobu kinatusaidia tukuwe sire asema ‘bya kweri tu, Mungu ashiwezi kufanya mambo ya mubaya.’ (Soma Yobu 34:12.) Kitabu kya Yobu kinatufundisha nju ya nini Mungu anachaka mateso, na vile tunezi kuivumilia. Na kinatusaidia kupachia nguvu bale beko nateswa. Mu abari ile iko nafwata, tutaona vile kitabu kya Yobu kinezi kutusaidia kuleta mashauri ya muzuri.
MWIMBO 156 Kwa Imani
a Pengine Yobu ariishi kisha Joseph kufwa na mbele Jeova amuchakule Moïse nju ya kuongoza batoto ba Israel. Iko sa ni mu ile wakati njo Shetani arianza kubishana na Jeova nju ya Yobu na njo wakati Yobu aripata mateso.
b Turishanjé manjina ingine.