MAMBO ILE UNEZI KUFUNDA
Ukuwe sire asema Jeova eko na nguvu ya kukuokoa
Soma Hesabu 13:25–14:4 nju uone vile batoto ba Israel barikosaka kumutumainia Jeova.
Tafuta kuyuwa vile mambo irikuwaka. Ni nini iripashwaka kusaidia batoto ba Israel saa barianzaka kutoka mu Égypte batumainie ya kusema Jeova eko na nguvu ya kubaokoa? (Zb. 78:12-16, 43-53) Sasa ni nini irifanyaka bashiendelee kumutumainia Jeova? (Kum. 1:26-28) Josué na Caleb barioneshaka je asema barimutumainia Jeova?—Hes. 14:6-9.
Ingia sasa ndani. Batoto ba Israel baripashwaka kufanya nini nju bamutumainie sana Jeova? (Zb. 9:10; 22:4; 78:11) Nju tufikie kumutumainia Jeova, nju ya nini tunapashwa mbele kumweshimia?—Hes. 14:11.
Unafunda nini? Uriulize ivi:
‘Ni mambo kani ile inezi kufanya nishimutumainie Jeova sana?’
‘Minezi kufanya nini nju nimutumainie sana Jeova leo na mu mashiku ile iko nakuya?’
‘Saa mateso ya nguvu sana itanza, minapashwa kuwa sire na nini?’—Luka 21:25-28.