Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w14 1/8 uku. 5
  • Mungu Anakuelewa

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Mungu Anakuelewa
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Mungu Anakuelewa?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2018
  • Tuliumbwa kwa Njia ya Ajabu
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2016
  • “Ee Yehova, . . . Unanijua”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Itika Musamaha wa Yehova
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
w14 1/8 uku. 5

KICHWA | MUNGU ANAKUONA

Mungu Anakuelewa

“Ee Yehova, umenichunguza kabisa, nawe unanijua.” —ZABURI 139:1.

ADN na kiini-tete

““Macho yako yalikiona kiini-tete changu.” —ZABURI 139:16

SABABU INAYOFANYA WATU FULANI WAWE NA MASHAKA: Watu fulani wanafikiri kwamba Mungu anaona wanadamu kuwa tu wenye zambi, ni kusema, wasiokuwa safi na wasiostahili kuhangaikiwa naye. Kendra, ambaye alisumbuliwa na hali ya kuvunjika moyo, alijisikia kuwa mwenye makosa sana kwa sababu hakuweza kutimiza kabisa mambo Mungu anataka. Kwa hiyo, alisema hivi: “Niliacha kusali.”

MAMBO NENO LA MUNGU LINAFUNDISHA: Yehova hakazie uangalifu makosa yako na anaelewa namna uko kabisa. Biblia inasema hivi: “Analijua vema umbo letu, akikumbuka kwamba sisi ni mavumbi.” Zaidi ya hilo, hatutendee ‘kulingana na zambi zetu’ lakini anatusamehe kwa rehema wakati tunatubu.—Zaburi 103:10, 14.

Fikiria Daudi, mufalme wa Israeli aliyetajwa katika habari ya kwanza. Katika sala, Daudi alimuambia Mungu hivi: “Macho yako yalikiona kiini-tete changu, na katika kitabu chako sehemu zake zote zilikuwa zimeandikwa . . . Unichunguze kabisa, Ee Mungu, uujue moyo wangu.” (Zaburi 139:16, 23) Kwa kweli, Daudi alikuwa na uhakika kwamba hata ikiwa alifanya zambi, hata zambi nzito wakati fulani, Yehova angetambua moyo wake wenye kutubu.

Yehova anakuelewa vizuri kuliko namna mwanadamu yeyote anakuelewa. Biblia inasema hivi: ‘Mwanadamu anaona kile kinachoonekana kwa macho, lakini Yehova anaona jinsi moyo ulivyo.’ (1 Samweli 16:7) Mungu anajua ni nini inayokufanya utende kwa njia fulani, ni kusema, anajua namna mambo kama vile hali uliyoriti, namna ulikomaa, mazingira yako, na tabia yako, yanakufanya uwe namna uko. Anaona na anapendezwa na namna unajikaza kuwa, hata ikiwa unafanya makosa.

Hata hivyo, namna gani Mungu anatumia uelewaji wake mwingi wa ‘namna uko kabisa’ ili kukufariji?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine