Tutoe Habari Njema, Tukitambua Kwamba Wakati Unasonga Mbele
1 Tunaonyesha shukrani yetu kwa ajili ya tumaini la Ufalme wa Mungu kwa kushiriki kwa moyo wote katika huduma ya Kikristo. Tunapaswa kuishiriki tukiwa wenye kutambua kwamba wakati unasonga mbele. Kwa nini? Wafanyakazi ni wachache, mwisho wa mfumo wa mambo mwovu unakaribia na uzima wa watu wa eneo ni katika hatari. (Ezek. 3:19; Mt. 9:37, 38) Daraka kubwa kama hili linaomba kwamba tufanye sote bidii yetu yote katika huduma. Jinsi gani tunaweza kuonyesha kwamba sisi tunatambua uharaka wa nyakati katika mahubiri? Kwa kutayarisha matangulizi mazuri, kwa kutafuta kwa juhudi watu popote wanakopatikana, kwa kuandika hasa kupendezwa kokote kulikoonyeshwa, kwa kufanya haraka ziara za kurudia ili kukuza kupendezwa huko na kwa sisi kukumbuka kwamba, kwa kuwa uzima wa watu ni katika hatari, tungepaswa kuchukua huduma yetu kwa uzito. Madokezo yafuatayo yataweza kuwa yenye manufaa wakati tutakapojitayarisha kutoa habari njema mnamo Machi, tukitambua kwamba wakati unasonga mbele. Tutatolea kitabu Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
2 Labda tungeweza kuanzisha mazungumzo kwa kutaja kwa kifupi matatizo yale yale yanayowapata majirani, kwa kusema:
◼ “Watu wengi wanaamini katika Mungu, lakini wanajiuliza ni wakati gani ujao anatuandalia. Unafikiri nini? [Tuache mtu ajibu.] Je! unajua kwamba Biblia inatueleza waziwazi juu ya mapenzi ya Mungu kuelekea wanadamu na yale ambayo anafanya sasa ili kuyatimiza?” Tufungue kitabu Upeo wa Ufunuo kwenye ukurasa 301. Tusome katika fungu la kwanza Ufunuo 21:1, na pia mafasirio yake katika sehemu ya pili ya fungu la 2. Tuonyeshe picha ya ukurasa 302 inayoonyesha jinsi hilo linavyomaanisha kuhusu wakati wetu ujao. Katika fungu la 6, tunasoma Ufunuo 21:4. Ikiwa mtu anaitikia vizuri, tumtolee kitabu kwa mchango mdogo unaolingana. Tupatane wakati wenye kufaa ili kuendeleza mazungumzo baadaye.
3 Tungeweza kurudilia mazungumzo juu ya Ufunuo 21:1, 4 hivi:
◼ “Mara ya mwisho nilipokuja, tulizungumzia ahadi ya Mungu ya kutayarisha jamii mpya ya wanadamu duniani. [Tuvutie tena uangalifu juu ya ukurasa 302 wa kitabu Upeo wa Ufunuo.] Je! ungependa kwamba familia yako ifaidike na hali kama hizi? [Tuache mtu ajibu.] Ulizo linajitokeza: Je! ahadi za Mungu zinastahili kuaminiwa? Angalia yale aliyoyasema mwenyewe.” Tusome Ufunuo 21:5, 6a kwenye fungu la 8 la ukurasa 303. Tuulize ulizo la fungu la 9, kwenye ukurasa 304, na tusome jibu, kutia ndani sentensi ya mwisho ya fungu. Tutolee funzo la bure la Biblia. Tuchukue mipango ili kufanyia hilo onyesho baadaye.
4 Watu wengi wanahangaishwa na ongezeko la matatizo ambayo wanadamu wanapambana nayo; pia tungeweza kusema, wakati wa ziara yetu ya kwanza, kitu fulani kama:
◼ “Watu walio wengi wanahangaishwa na matatizo ambayo yanatushambulia. [Taja mojawapo yayo.] Kumepita hivyo makumi ya miaka ambayo wanasiasa wanaahidi kumaliza kabisa kabisa matatizo, na wamoja walijaribu kufanya hivyo. Kulingana nawe, kwa nini hali inaendelea kuwa yenye hatari. [Tuache mtu ajibu.] Biblia inatoa mafasirio ambayo watu wengi hawajachunguza kamwe. Kitabu cha Ufunuo kinaeleza vita fulani iliyofanyika mbinguni. Angalia jinsi mwisho ulivyokuwa, kulingana na Ufunuo 12:9.” Tusome andiko na tufungue kitabu Upeo wa Ufunuo kwenye ukurasa 182. Tutumie picha ili kuonyesha jinsi Shetani anavyojiingiza katika mambo ya wanadamu. Tuchukue uamuzi wa kumtolea kitabu. Tuagane ili kurudi tena kumuonyesha jinsi Mungu atakavyotatua matatizo ya wanadamu.
5 Ikiwa tuliahidi kurudi kuonyesha soluhisho ambalo Mungu atatoa kwa matatizo ya sasa, tungeweza kujaribu kusema:
◼ “Nimerudi hasa kuja kukuona ili tuendeleze mazungumzo yetu juu ya suluhisho la kweli kwa matatizo ya wanadamu. Mara ya mwisho, tuliona katika Biblia kwamba Shetani anadanganya dunia yote inayokaliwa na watu. Kwa kuwa yeye ni kiumbe cha kiroho chenye nguvu kuliko mwanadamu, je! unafikiri kwamba kuna njia ya kukatilia mbali uvutano wake mwovu? [Tuache mtu ajibu.] Angalia yale Biblia inavyosema juu ya hilo.” Tusome na tufasirie Ufunuo 20:1-3. Kwa msaada wa picha za kurasa 4 na 5 za kitabu Ujuzi, tuonyeshe hali za maisha zitakuwaje wakati uvutano wa Shetani utakapokoma. Tutolee funzo la Biblia na tujaribu kulianzisha papo hapo.
6 Watu wengi wanapendezwa na mazingira. Tungeweza hivyo kujaribu kuanzisha mazungumzo kwa namna ifuatayo:
◼ “Tunaona kwamba karibu kila mtu anahangaishwa na uchafuzi wa hewa, wa maji na wa chakula. Katika nchi fulani, hali ya mazingira inahatarisha hata uhai. Kwa kuwa Mungu ndiye Muumba wa dunia, atafanya nini kulingana nawe? [Tuache mtu ajibu.] Biblia inasema kwamba Mungu ataomba hesabu kwa wanadamu kwa namna ambayo wanaitumia dunia. [Tusome Ufunuo 11:18b.] Fikiria kwamba unaishi katika dunia isiyokuwa na uchafuzi wowote wa mazingira! Onyesha ahadi ambayo Mungu anafanya kuhusu paradiso katika Ufunuo 21:3, 4. Tuonyeshe picha ya ukurasa 302 ya kitabu Upeo wa Ufunuo. Ikiwa kupendezwa ambako mtu anaonyesha kunatusukuma, tumtolee kitabu na tuchukue mipango ili kurudi kumuona tena.
7 Kwa kurudi kumuona mtu aliyeonyesha kupendezwa na Paradiso duniani, tunaweza kusema:
◼ “Mara ya mwisho, tulikubaliana kusema kwamba itafaa Mungu aingilie kati katika mambo ya wanadamu ili kutengeneza tatizo la uchafuzi wa dunia. Lakini ulizo linajitokeza: tunapaswa kufanya nini ili kuishi katika ulimwengu mpya na wa haki wa Mungu? Tusome Yohana 17:3. Tumualike msikilizaji kufaidika na funzo la Biblia la bure linalowezesha kupata ujuzi huo wa pekee.
8 Ni pendeleo kama nini kwetu kuweza kutumiwa kama wafanyakazi katika mavuno yanayofanyika leo, na kushiriki katika kazi ya kuhubiri ambayo inaokoa uhai! Sote tuwe wenye kushughulika kutolea habari njema, huku tukitambua kwamba wakati unasonga mbele na ‘tukijua kwamba kazi yetu ya jasho si bure.’—1 Cor. 15:58, TUM.