Majibu Kwa Maulizo Yenu
◼ Nini la kufanya ikiwa kunatokea maafa yanayowapata moja kwa moja ndugu zetu?
Ikiwa Maafa Yanatokea Katika Eneo Lenu: Usiogope. Tulia na kaza akili juu ya mambo ya lazima: uhai, si vitu vya kimwili. Toa msaada wa kimwili papo hapo ambao familia yako inahitaji. Kisha julisha wazee hali yako ipo namna gani na ni wapi unapatikana.
Wazee na watumishi wa huduma wanatimiza daraka la maana katika kutayarisha misaada. Ikiwa ajali inatangazwa, kama inavyokuwa na pepo kali, ndugu hao watahakikisha kwamba watu wote wanapatikana mahali salama na, ikiwa wana wakati, watajipatia chakula na watakigawanya.
Baadaye, viongozi wa funzo la kitabu wangepaswa kujua mahali kila familia ilipo na kutafuta kujua hali yayo. Tungepaswa kumjulisha mwangalizi-msimamizi au mzee mwingine ni nini hali ya kila familia, hata ikiwa mambo yote yanakwenda vema. Ikiwa mtu anaumia, wazee watajikaza kuchukua mipango ili kwamba apate matunzo. Watatoa pia vitu vyote vya kimwili vya lazima: chakula, mavazi, nyumba au bidhaa ya nyumbani, kwa mfano. (Yn. 13:35; Gal. 6:10) Ikiwa hali ni mbaya hivi kwamba ni lazima kutoka katika mtaa, kama ilivyokuwa hivi karibuni katika Mashariki mwa Zaïre, ingekuwa vizuri zaidi ndugu wabaki pamoja, chini ya uongozi na ulinzi wa mmoja wa wazee. Si jambo la hekima kwamba familia zitengane na kutawanyika huku na huku. Wazee wa mtaa watawatolea tegemezo la kiroho na la kiakili kwa kutaniko na, tangu tu inapowezekana, watajikaza kupanga tena mikutano. Baada ya uchunguzi wa makini wa hali, mzee mmoja angepaswa, kwa niaba ya baraza, kwenda kumuona mwangalizi wa mzunguko ili kumjulisha ikiwa kuna majeruhi (waliyoumia), vitu vilivyoharibika kwenye Jumba la Ufalme au kwenye nyumba za akina ndugu, na pia mahitaji ya pekee. Mwangalizi wa mzunguko atapiga hivyo simu kwenye tawi ili kuripoti juu ya hali hiyo. Ikiwa inaomba kuchukua maamuzi makubwa, tawi litasimamia misaada.
Ikiwa Maafa Yanatokea Katika Eneo Lingine: Tukumbuke ndugu na dada zetu katika sala zetu. (2 Kor. 1:8-11) Ikiwa tunataka kuwapelekea msaada wa kifedha, tunaweza kutuma michango yetu kwenye Sosaiti ambayo inalinda fedha za misaada inayotayarishwa mapema kwa kusudi hilo. Angalieni anwani: Association “Les Témoins de Jéhovah”, B.P. 634, Limete-Kinshasa, Zaïre. (Mdo. 2:44, 45; 1 Kor. 16:1-3; 2 Kor. 9:5-7; ona Mnara wa Mlinzi wa Desemba 1, 1985, kur. 20-2 [Kifaransa].) Msitume wala bidhaa wala vitu katika eneo lenye maafa, isipokuwa tu ikiwa ndugu wanaopanga misaada wanawaomba kufanya hilo haraka. Hivyo misaada itatolewa kwa namna ya utaratibu, na itagawanywa vizuri. (1 Kor. 14:40) Tafadhali msipigie Sosaiti simu pasipo sababu, kwani hilo lingeweza kujaza njia za simu za lazima kwa kupokea miito inayotoka katika eneo lenye maafa.
Baada ya uchunguzi mzuri wa hali, Sosaiti itaamua ikiwa ni lazima kuunda halmashauri ya msaada. Ndugu wanaopaswa kutumikia daraka hilo watapaswa kujulishwa. Kila mmoja angepaswa kushirikiana na wazee wanaoongoza mambo ili kwamba mahitaji ya ndugu wote yaweze kutoshelezwa kama inavyopaswa. —Ona kitabu Les Témoins de Jéhovah : Prédicateurs du Royaume de Dieu, kur. 310-15.