Ukumbusho—Tukio La Maana Sana
1 Siku ya Yenga Machi 23, kisha kutua kwa jua, tutaadhimisha kifo cha Kristo. (Lk. 22:19) Bila shaka, tukio hilo ni la maana zaidi! Kwa kulinda ushika-ukamilifu wake kwa Yehova hadi kufikia kifo, Yesu alionyesha kwamba inawezekana kwa mwanadamu kubaki mshikamanifu kikamilifu kwa Mungu hata katika hali yenye majaribu, tukitetea hivyo uhalali wa Enzi Kuu ya Yehova. (Ebr. 5:8) Zaidi ya hilo, kupitia kifo chake Kristo alitoa dhabihu kamilifu ya kibinadamu ya lazima ili kuwakomboa wanadamu, akitoa uwezekano kwa wale wanaoonyesha imani ya kuishi milele. (Yn. 3:16) Kwa kuwapo kwetu kwenye Ukumbusho, tunaonyesha shukrani yetu kubwa kwa upendo wa Yehova na kwa dhabihu ya Yesu kwa faida yetu.
2 Sisi sote tunatiwa moyo kufuata programu ya usomaji wa Biblia unaotayarishwa mapema tangu Machi 18 mpaka 23 na unaopatikana kwenye Kalenda ya Mashahidi wa Yehova 1997. Kwa upande mwingine, mazungumzo katika familia ya sura 112-16 za kitabu Yule Mtu Mkubwa Zaidi Aliyepata Kuishi yatatusaidia kukaza akili juu ya juma la maana zaidi la historia yote.
3 Je! tunaweza kuongeza kushiriki kwetu katika mahubiri wakati wa Ukumbusho? Mnamo Machi, wahubiri wengi watafaidika kikamilifu na miisho-juma tano ili kuwa mapainia wasaidizi. Kwa nini wewe pia usifanya hivyo? Tunaweza sote kufanya mengi ili kuonyesha watu umaana wa kuhudhuria kwenye Ukumbusho. Kwa kuwa unaanguka Siku ya Yenga, itakuwa rahisi zaidi, kwa walio wengi, kuudhuria. Tuangalie ili kualika wale wote wanaojifunza Biblia na pia watu wengine walio na mwelekeo mzuri. Tuzungumze pamoja nao juu ya yale yanayosemwa kwenye ukurasa 127 wa kitabu Ujuzi, fungu 18, kuhusu mwadhimisho ambao unapaswa kuadhimishwa kila mwaka.
4 Tuthamini tukio hilo, la maana zaidi la 1997, tukiwa wenye kutambua kabisa yale kifo cha Yesu kinamaanisha kwetu. Tuwepo katika jioni hiyo ya Machi 23 ambako Wakristo wa kweli wa ulimwenguni pote wataadhimisha kiaminifu Ukumbusho.