18
Muti Mudogo Unawaka Moto
Musa alifanya miaka 40 kule Midiani. Alioa na kuzaa watoto. Siku moja wakati alikuwa anachunga kondoo zake karibu na Mulima Sinai, aliona jambo la kushangaza. Muti ulikuwa unawaka moto bila kuungua! Wakati alienda karibu juu aone muzuri, alisikia sauti inatoka mu ule muti na kusema: ‘Musa! Usikaribie. Tosha viatu, juu mahali kwenye umesimama ni patakatifu.’ Yehova njo alikuwa anasema kupitia malaika.
Musa aliogopa, kwa hiyo akaficha uso wake. Ile sauti ikasema: ‘Nimeona mateso ya Waisraeli. Nitawakomboa kutoka Misri na kuwapeleka mu inchi ya muzuri. Na ni wewe njo utatosha watu wangu mu inchi ya Misri.’ Hauone kama jambo hilo lilishangaza Musa?
Musa akauliza: ‘Wakati wataniuliza kama nani njo alikutuma, nitawaambia nini?’ Mungu akamujibu: ‘Uwaambie kama Yehova, Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaka, Mungu wa Yakobo njo mwenye amekutuma.’ Kisha Musa akauliza: ‘Itakuwa namna gani kama wale watu hawanisikilize?’ Yehova alifanya mambo fulani ya kumuonyesha kama atamusaidia. Aliambia Musa atupe fimbo yake chini. Kisha ile fimbo ikakuwa nyoka! Wakati Musa alikamata ile nyoka ku mukia, ikageuka tena fimbo. Yehova akamuambia: ‘Wakati utafanya huu muujiza, watajua kama mimi njo nilikutuma.’
Musa akasema: ‘Mimi sijue kusema muzuri.’ Yehova akamuambia: ‘Nitakuambia mambo yenye utasema, na nitatuma Haruni, ndugu yako akusaidie.’ Musa alijua kama Yehova iko pamoja naye. Kwa hiyo, alikamata bibi yake na watoto wake, na wakarudia Misri.
“Musihangaike juu ya mambo yenye mutasema ao namna mutayasema, kwa sababu mutapewa mambo ya kusema saa hiyo.”—Matayo 10:19