Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • lfb somo 18 uku. 48-uku. 49 fu. 4
  • Muti Mudogo Unawaka Moto

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Muti Mudogo Unawaka Moto
  • Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Musa​—Mwanaume Aliyeonyesha Upendo
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Tuige Imani ya Musa
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Musa Alikuwa Nani?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Macho Yako Yanaangalia Wapi?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2018
Ona Habari Zaidi
Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
lfb somo 18 uku. 48-uku. 49 fu. 4
Musa iko karibu na muti wenye kuwaka moto

18

Muti Mudogo Unawaka Moto

Musa alifanya miaka 40 kule Midiani. Alioa na kuzaa watoto. Siku moja wakati alikuwa anachunga kondoo zake karibu na Mulima Sinai, aliona jambo la kushangaza. Muti ulikuwa unawaka moto bila kuungua! Wakati alienda karibu juu aone muzuri, alisikia sauti inatoka mu ule muti na kusema: ‘Musa! Usikaribie. Tosha viatu, juu mahali kwenye umesimama ni patakatifu.’ Yehova njo alikuwa anasema kupitia malaika.

Musa aliogopa, kwa hiyo akaficha uso wake. Ile sauti ikasema: ‘Nimeona mateso ya Waisraeli. Nitawakomboa kutoka Misri na kuwapeleka mu inchi ya muzuri. Na ni wewe njo utatosha watu wangu mu inchi ya Misri.’ Hauone kama jambo hilo lilishangaza Musa?

Musa akauliza: ‘Wakati wataniuliza kama nani njo alikutuma, nitawaambia nini?’ Mungu akamujibu: ‘Uwaambie kama Yehova, Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaka, Mungu wa Yakobo njo mwenye amekutuma.’ Kisha Musa akauliza: ‘Itakuwa namna gani kama wale watu hawanisikilize?’ Yehova alifanya mambo fulani ya kumuonyesha kama atamusaidia. Aliambia Musa atupe fimbo yake chini. Kisha ile fimbo ikakuwa nyoka! Wakati Musa alikamata ile nyoka ku mukia, ikageuka tena fimbo. Yehova akamuambia: ‘Wakati utafanya huu muujiza, watajua kama mimi njo nilikutuma.’

Musa akasema: ‘Mimi sijue kusema muzuri.’ Yehova akamuambia: ‘Nitakuambia mambo yenye utasema, na nitatuma Haruni, ndugu yako akusaidie.’ Musa alijua kama Yehova iko pamoja naye. Kwa hiyo, alikamata bibi yake na watoto wake, na wakarudia Misri.

“Musihangaike juu ya mambo yenye mutasema ao namna mutayasema, kwa sababu mutapewa mambo ya kusema saa hiyo.”​—Matayo 10:19

Maulizo: Musa aliona nini wakati alikuwa anachunga kondoo zake? Yehova aliomba Musa afanye nini?

Kutoka 3:1–4:20; Matendo 7:30-36

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine