Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • lfb somo 64 uku. 152-uku. 153 fu. 4
  • Danieli Anatupwa Ndani ya Shimo la Simba

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Danieli Anatupwa Ndani ya Shimo la Simba
  • Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Tujifunze Mambo Fulani Kupitia Mufano wa Danieli
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2023
  • Je, Kweli Mungu Anakujali?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
lfb somo 64 uku. 152-uku. 153 fu. 4
Wanaume wenye wivu wanakuta Danieli na iko anasali mbele ya dirisha lenye kuwa wazi

64

Danieli Anatupwa Ndani ya Shimo la Simba

Mufalme mwingine wa Babiloni alikuwa Dario Mumedi. Alitambua kama Danieli hakukuwa sawa na watu wengine. Alimuweka Danieli kuwa mukubwa wa watu wake wa maana sana mu inchi. Wale watu walisikilia Danieli wivu na walitaka kumuua. Walijua kama Danieli alizoea kusali kwa Yehova mara tatu kila siku. Basi waliambia Dario: ‘Ee mufalme, inafaa kukuwe sheria yenye kuomba kila mutu akuwe anatoa sala kwako tu. Kama mutu fulani hatii ile sheria anapaswa kutupwa ndani ya shimo la simba.’ Dario alifurahia wazo hilo na akatia sinyatire yake ku ile sheria.

Wakati tu Danieli alipata habari juu ya ile sheria ya mupya, akaenda kwake. Akapiga magoti mbele ya dirisha lake lenye lilikuwa wazi, na akaanza kusali kwa Yehova. Wale wanaume wenye walikuwa wanamusikilia Danieli wivu waliingia mu nyumba yake na kumukuta iko anasali. Mara moja wakaenda haraka kwa Dario na kumuambia: ‘Danieli hatii sheria yako. Iko anasali kwa Mungu wake mara tatu kila siku.’ Dario alikuwa anamupenda Danieli, na hakupenda akufe. Siku muzima alikuwa anawaza atafanya nini ili kumuokoa Danieli. Lakini hata mufalme hakukuwa na ruhusa ya kubadilisha sheria yenye yeye mwenyewe alikuwa ametia sinyatire. Dario alilazimika kupatia watu wake amri ya kutupa Danieli ndani ya shimo mwenye mulikuwa simba wakali.

Ule usiku, Dario alikuwa na wasiwasi sana juu ya Danieli na hakuweza kulala usingizi. Asubui, alienda mbio kwenye shimo la simba na kuuliza Danieli: ‘Mungu wako alikuokoa?’

Dario akasikia sauti. Ilikuwa sauti ya Danieli! Danieli akamujibu Dario: ‘Malaika wa Yehova alifunga vinywa vya simba. Hawakuniumiza hata kidogo.’ Dario alifurahi sana! Akatoa amri watoshe Danieli ndani ya ile shimo. Simba hawakumuumiza Danieli hata kidogo. Kisha mufalme akatoa amri hii: ‘Mutupe ndani ya shimo la simba wanaume wenye walimushitaki Danieli.’ Wakati walitupa wale wanaume ndani ya shimo, mara moja simba wakawakula.

Dario alitumia watu wake wote amri hii: ‘Kila mutu anapaswa kuogopa Mungu wa Danieli juu alimuokoa Danieli ndani ya shimo la simba.’

Na wewe, unazoea kusali kwa Yehova kila siku kama Danieli?

Danieli iko ndani ya shimo la simba

“Yehova anajua namna ya kukomboa kutoka katika jaribu watu wenye ushikamanifu kwa Mungu.”​—2 Petro 2:9

Maulizo: Danieli alizoea kufanya nini mara tatu kila siku? Yehova alifanya nini ili kumuokoa Danieli?

Danieli 6:1-28

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine