Maulizo Juu Ya Habari Za Biblia Yanajibiwa
Sababu gani Kristo atarudia?
Mbele Yesu Kristo apande kuenda mbinguni katika mwaka wa 33, aliahidi kwamba atarudia. Alijifananisha na tajiri ambaye alisafiri kwa muda murefu na wakati alirudia alikuwa na mamlaka ya kutawala akiwa mufalme. Yesu atarudia ili kuwaletea wanadamu serikali nzuri.—Soma Luka 19:11, 12.
Yesu atawaletea wanadamu serikali nzuri
Kristo atarudia katika mwili wa aina gani? Alifufuliwa akiwa mutu wa roho asiyeonekana. (1 Petro 3:18) Kisha, akaenda mbinguni na akakaa kwenye mukono wa kuume wa Mungu. (Zaburi 110:1) Miaka mingi baadaye, Yesu aliletwa mbele ya Yehova Mungu, ‘Muzee wa Siku,’ ambaye alimupatia mamlaka ya kutawala wanadamu. Kwa hiyo, Yesu hatarudia katika mwili wa kibinadamu, lakini atarudia kama Mufalme asiyeonekana.—Soma Danieli 7:13, 14.
Yesu atafanya nini atakaporudia?
Wakati Yesu atarudia bila kuonekana pamoja na malaika zake, atawahukumu wanadamu. Ataharibu watu waovu na kuwapatia uzima wa milele wale ambao wanamukubali kuwa Mufalme.—Soma Mathayo 25:31-33, 46.
Utawala wa Yesu akiwa Mufalme utageuza dunia hii kuwa paradiso. Atafufua watu waliokufa ili wafurahie maisha katika dunia hii itakayokuwa Paradiso.—Soma Luka 23:42, 43.