Kutolea Watu Vichapo Katika Eneo Ambamo Lugha Nyingi Zinasemwa
1 Mahali pengi, shamba linaanza kutia ndani watu kutoka nchi nyingine au majimbo mengine. Wengi wao hujifunza kweli kwa uharaka zaidi na kwa uelewevu wenye kina kirefu zaidi wanapofundishwa katika lugha yao ya asili. Ni mipango gani iliyopo ili wale wanaopendezwa waandaliwe vichapo vyenye kutegemea Biblia katika lugha wanayoielewa vizuri zaidi?
2 Wakati wa Kutolea Watu Vichapo: Wakati makutaniko mawili au zaidi yanayosema lugha tofauti yanapohubiri katika eneo lilelile, mabaraza ya wazee yanayohusika yatashirikiana na waangalizi wa utumishi katika kufanya mpango unaokubaliwa na kila kutaniko ili kila kikundi cha lugha kitolewe ushahidi kamili. Wanapohubiri nyumba kwa nyumba, kwa kawaida wahubiri hawatatolea watu vichapo katika lugha ya kutaniko au makutaniko yale mengine. Lakini, wahubiri wanapotoa ushahidi wa vivi hivi au wanapohubiri katika maeneo ya watu wote, wanaweza kutolea watu vichapo katika lugha za watu wa hapo.
3 Wakati wa Kuweka Vichapo Katika Stoki: Ni jambo gani linaloweza kufanywa ikiwa eneo lina watu wengi wanaosema lugha ya kigeni lakini hakuna kutaniko linalosema lugha hiyo hasa? Katika hali hizo, makutaniko yanaweza kuweka katika stoki kiasi kidogo cha vichapo vya msingi vinavyopatikana katika lugha hiyo, kama vile trakti, broshua Anataka na Rafiki ya Mungu, na kitabu Ujuzi. Wahubiri wanaweza kutolea watu vichapo hivyo wakati wowote wanapokutana na watu wanaosema lugha hiyo.
4 Jinsi ya Kufanya Ombi la Vichapo: Ikiwa kutaniko halina stoki ya vitabu katika lugha ambayo mtu anayependezwa anasoma, vichapo katika lugha hiyo vinaweza kupatikanaje? Mhubiri anapaswa kuuliza ndugu anayeshughulika na vichapo ili kujua ni vichapo gani vinavyopatikana katika lugha hiyo kusudi vichapo vinavyohitajiwa viombwe kwenye ombi lijalo la kutaniko.
5 Ikiwa mhubiri anahitaji kuhudumiwa kwa uharaka zaidi, anaweza kuuliza mshiriki mmoja wa Halmashauri ya Utumishi ya Kutaniko ikiwa ombi linaweza kutolewa kabla ya ombi lijalo la vichapo ambalo kutaniko linapanga kutoa. Ikiwa hilo linakubaliwa, msimamizi wa vichapo au mtu fulani anayechaguliwa naye anaweza kutuma ombi la haraka kupitia barua kwa ofisi ya tawi. Vichapo hivyo vitatumwa kupitia anwani ya kawaida ya kutaniko au anwani ya muda, ikiwa jambo hilo linatakiwa.
6 Na tutumie vizuri vichapo vya Kikristo ili kusaidia “watu wa namna zote,” hata lugha yao iwe nini, ‘waje kwenye ujuzi sahihi wa kweli.’—1 Tim. 2:3, 4.
[Study Questions]
1. Kwa nini makutaniko mengi yanahitaji vichapo katika lugha ya kigeni?
2. Ni ushirikiano gani unaohitajiwa wakati makutaniko mawili au zaidi yanayosema lugha tofauti yanapohubiri katika eneo lilelile?
3. Ni wakati gani kutaniko linaweza kuweka katika stoki vichapo katika lugha nyingine?
4. Vichapo katika lugha ambayo kutaniko haina katika stoki vinawezaje kupatikana?
5. Ni nini linaloweza kufanywa ikiwa vichapo vinahitajiwa kabla ya kupokea vichapo vinavyopatikana kwenye ombi lenu lijalo?
6. Mradi wetu ni nini katika kutoa vichapo vya Kikristo?