Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 12/03 uku. 1
  • Umoja wa Kweli Kati ya Wakristo—Jinsi Gani?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Umoja wa Kweli Kati ya Wakristo—Jinsi Gani?
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Ukumbusho Unaunganisha Watu wa Mungu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2018
  • Yehova Anakusanya Tena Familia Yake
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
Huduma Yetu ya Ufalme—2003
km 12/03 uku. 1

Umoja wa Kweli Kati ya Wakristo—Jinsi Gani?

1 Ni nini kinachoweza kuunganisha zaidi ya watu milioni sita kutoka nchi 234 na vikundi vya lugha 380? Ni ibada ya Yehova Mungu tu. (Mika 2:12; 4:1-3) Mashahidi wa Yehova wanajua kutokana na mambo wanayojionea kwamba umoja wa kweli wa Kikristo ni jambo halisi leo. Tukiwa “kundi moja” chini ya ‘mchungaji wetu mmoja,’ tunaazimia kukinza roho ya ulimwengu huu yenye kugawanya watu.—Yoh. 10:16; Efe. 2:2.

2 Kusudi hakika la Mungu ni kwamba uumbaji wote wenye akili uungane katika ibada ya kweli. (Ufu. 5:13) Kwa kuwa alijua umaana wa jambo hilo, Yesu alisali kwa bidii kuhusu umoja wa wafuasi wake. (Yoh. 17:20, 21) Kila mmoja wetu anawezaje kuchangia kufanya kutaniko la Kikristo liwe na umoja?

3 Jinsi Umoja Unavyofikiwa: Bila Neno la Mungu na roho yake, haingewezekana kufikia umoja wa Kikristo. Kutumikisha yale tunayosoma katika Biblia kunawezesha roho ya Mungu itende bila kizuizi maishani mwetu. Kunatuwezesha “kuushika umoja wa roho katika kifungo chenye kuunganisha cha amani.” (Efe. 4:3) Kunatuchochea tuvumiliane katika upendo. (Kol. 3:13, 14; 1 Pet. 4:8) Je, unaendeleza umoja kwa kutafakari Neno la Mungu kila siku?

4 Utume wetu wa kuhubiri na kufanya wanafunzi pia unatuunganisha. Tunapofanya kazi na wengine katika huduma ya Kikristo, ‘tukikazana pamoja kwa ajili ya imani ya habari njema,’ tunapata kuwa “wafanyakazi wenzi katika kweli.” (Flp. 1:27; 3 Yoh. 8) Tunapofanya hivyo, vifungo vya upendo vinavyotuunganisha katika kutaniko vinaimarishwa. Kwa nini usialike mtu fulani ambaye hukuhubiri naye majuzi aambatane nawe katika huduma ya shambani juma hili?

5 Sisi ni wenye pendeleo kama nini kuwa sehemu ya undugu pekee wa kweli na wa kimataifa duniani leo! (1 Pet. 5:9) Karibuni, maelfu walijionea wenyewe umoja huo wa ulimwenguni pote kwenye Mikusanyiko ya Kimataifa “Mtukuzeni Mungu.” Kila mmoja wetu na achangie kuendeleza umoja huo wenye thamani kwa kusoma Neno la Mungu kila siku, kwa kutatua kutoelewana kwa upendo, na kwa kuhubiri habari njema “kwa umoja.”—Rom. 15:6.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine