Kugawanyia Watu Mwaliko wa Ukumbusho Ulimwenguni Pote!
1. Ni kampanye gani ya pekee inayopangwa kufanywa ulimwenguni pote mbele ya Ukumbusho?
1 “Endeleeni kufanya hivi kwa kunikumbuka mimi.” (Luka 22:19) Kwa kutii amri hiyo ya Yesu, waabudu wa Yehova watakusanyika pamoja na watu wenye kupendezwa tarehe 30 mwezi wa 3, 2010, ili kuazimisha kifo cha Yesu. Kuanzia tarehe 13 mpaka tarehe 30 mwezi wa 3, tutagawia watu mwaliko wa pekee wa Ukumbusho ulimwenguni pote.
2. Namna gani tunaweza kumtolea mutu mwaliko?
2 Jinsi ya Kumtolea Mutu Mwaliko: Unaweza kumtolea mutu mwaliko mkononi ili aone picha iliyo kwenye ukurasa wa kwanza, kisha unaweza kuseme hivi: “Mangaribi ya tarehe 30 mwezi wa 3, mamilioni ya watu ulimwengu pote watakusanyika ili kuazimisha kifo cha Yesu. Nimekuja kukutolea wewe na familia yako mwaliko huu ili muje kuhuzuria. Unaweza pia kuja pamoja na marafiki zako.” Ikiwa hali inaruhusu, unaweza kumsomea Luka 22:19 ili aone andiko la Biblia linalotuamuru kukumbuka kifo cha Yesu, kumwonyesha pia wakati, na mahali ambapo Ukumbusho utafanywa katika eneo lenu. Hata hivyo, tukumbuke kwamba tunapaswa kusema maneno machache kwa kuwa wakati ni mdogo ili kila mutu katika eneo lenu lote apate mwaliko wake.
3. Ni watu gani tunaoweza kualika?
3 Ikiwa kutaniko lenu lina eneo kubwa, wazee wanaweza kuamua muache mialiko mahali ambapo hamukute watu nyumbani munapofika kwa mara ya kwanza. Mutolee watu magazeti pamoja na mwaliko, inapofaa. Musisahau kualika watu munaorudilia, watu munaojifunza nao Biblia, wafanyakazi wenzenu, wanafunzi wenzenu, watu wa jamaa, majirani, na watu wengine munaofahamiana nao.
4. Ili kuonyesha shukrani kwa ajili ya upendo ambao Yehova alionyesha kwa kutoa zabihu ya ukombozi, tutafanya nini?
4 Jitayarishe Ili Kushiriki Kabisa: Kipindi cha Ukumbusho ni wakati mzuri sana ili kushiriki zaidi katika kazi ya kuhubiri. Je, unaweza kubadili programu yako ili kuwa painia msaidizi? Je, una watoto ao wanafunzi wa Biblia wanaofanya maendeleo ya kiroho? Ikiwa ni hivyo, ongea na wazee ili waone ikiwa wanastahili kuwa wahubiri wasiobatizwa ili kushiriki katika kampanye hiyo ya pekee. Ili kuonyesha shukrani kwa ajili ya upendo ambao Yehova alionyesha kwa kutoa zabihu ya ukombozi, tutahuzuria Ukumbusho na pia tutaalika watu wengi zaidi waje kuhuzuria pamoja nasi.—Yoh. 3:16.