Kampanye ya Kuwaalika Watu Kwenye Ukumbusho Itaanza Tarehe 17 Mwezi wa 3
1. Ni kampanye gani itakayoanza tarehe 17 mwezi wa 3?
1 Kila mwaka tunafanya Ukumbusho ili kutangaza kifo cha Yesu. (1 Kor. 11:26) Kwa hiyo, tunataka wengine waje kuhuzuria sherehe hiyo pamoja nasi ili wajifunze kuhusu zabihu ya ukombozi ambayo ni zawadi inayoonyesha upendo wa Yehova. (Yoh. 3:16) Mwaka huu, kampanye hiyo itaanza Siku ya Posho, tarehe 17 mwezi wa 3. Je, umeanza kujitayarisha ili uhubiri kadiri uwezavyo wakati wa kampanye hiyo?
2. Tunaweza kusema nini tunapomutolea mutu mualiko?
2 Yale Tunayoweza Kusema: Ni vizuri zaidi kusema mambo machache. Tunaweza kusema hivi: “Jambo. Tunafika hapa ili kukualika wewe na familia yako kwenye tukio la maana linalofanywa ulimwenguni pote kila mwaka. Mwaka huu jambo hilo litafanywa tarehe 5 mwezi wa 4. Hotuba yenye kutegemea Biblia itatolewa, na itazungumuzia yale ambayo kifo cha Yesu kilitimiza na yale ambayo Yesu anafanya sasa. Kuingia ni bila malipo. Mwaliko huu unaonyesha saa na mahali mukutano huo utafanyika katika eneo lenu.” Tunapowagawanyia watu mialiko ya Ukumbusho Siku ya Posho ao Siku ya Yenga, tusisahau kuwatolea magazeti inapofaa.
3. Tutafanya nini ili tuwaalike watu wengi kadiri tuwezavyo?
3 Tuwaalike Watu Wengi Kadiri Tuwezavyo: Kusudi letu ni kuwaalika watu wengi kadiri tuwezavyo. Kwa hiyo, ufanye mipango ili kuwaalika watu unaojifunza nao Biblia, watu unaorudilia, watu wa jamaa, wafanyakazi wenzako, wale unaosoma nao, majirani, na watu wengine unaofahamiana nao. Wazee wa kutaniko watawajulisha kile munapaswa kufanya ili kuwatolea watu mialiko katika eneo lenu lote. Kampanye tunayofanya kila mwaka kuhusu Ukumbusho ili kualika watu ni yenye kuzaa matunda. Kwa mufano, mwaka uliopita mwanamuke mumoja alipoingia katika Jumba la Ufalme, ndugu aliyekuwa akikaribisha wageni alitaka kumusaidia ili akae pamoja na muhubiri aliyemualika. Lakini, mwanamuke huyo alimuambia kwamba hajui mutu yeyote, na kwamba alipewa mualiko na Shahidi aliyekuwa akigawanya mialiko nyumba kwa nyumba asubuhi hiyo.
4. Tuna sababu gani za kuhubiri kwa bidii wakati wa kampanye?
4 Labda mutu fulani uliyeachia mualiko atahuzuria Ukumbusho mahali penu. Iwe mutu uliyealika atafika ao hapana, hata hivyo, jua kwamba ushahidi umetolewa kupitia bidii yako. Mialiko utakayotolea watu itawajulisha kwamba leo hii Yesu ni Mufalme mwenye nguvu. Kuhubiri kwa bidii wakati wa kampanye kutawaonyesha wale wanaokutazama, yaani, watu wa eneo lenu, wahubiri wenzetu, na hasa, Yehova, kwamba unapendezwa kabisa na zawadi ya zabihu ya ukombozi.—Kol. 3:15.