HABARI JUU YA MAISHA YA WATU
“Sasa Napenda Mahubiri!”
NILIKOMALIA mu Nouvelle-Zélande, katika muji wa Balclutha. Wakati nilikuwa mutoto, nilimupenda Yehova na nilijisikia muzuri kuwa katika kweli. Mikutano haikukuwa inanichokesha, na nilijisikia muzuri na salama mu kutaniko. Hata kama nilikuwa mutu wa haya, nilifurahia kuhubiri kila juma. Sikuogopa kuhubiria wanafunzi wenzangu na watu wengine. Nilifurahia kuwa Shahidi wa Yehova, na wakati nilikuwa na miaka 11, nilitoa maisha yangu kwa Mungu.
NILIPOTEZA FURAHA YANGU
Wakati nilikuwa na miaka 13 hivi, urafiki wangu wa karibu sana pamoja na Yehova ulianza kufifia. Niliona kama wanafunzi wenzangu walikuwa na uhuru zaidi kuliko miye. Na miye nilipenda kuwa na uhuru zaidi, lakini niliona kama sheria zenye wazazi wangu walinipatia na kanuni za Kikristo zilinifunga sana. Na niliona mambo ya kiroho inakuwa muzigo. Sikukuwa na mashaka kama Yehova anakuwaka, lakini nilikuwa sijisikie tena kuwa karibu naye.
Nilikuwa nahubiri, lakini hapana tu sana. Nilikuwa naenda mu mahubiri bila kujitayarisha. Njo maana ilikuwa nguvu kwangu kuanzisha ao kuendelea na mazungumuzo, na ile ilifanya nisikuwe na matokeo ya muzuri mu mahubiri, nipoteze furaha, na ku mwisho nipoteze hamu ya kuhubiri. Kisha niliwaza, ‘Kuhubiri kila juma, kila mwezi, mbona ni bya nguvu!’
Wakati nilikuwa na miaka 17, nilipenda kuwa huru. Kisha nikafunga mizigo yangu, nikatoka kwetu na nikaenda Australia. Wazazi wangu walihuzunika sana wakati nilitoka kwetu, lakini walitumaini kama ningeendelea kumutumikia Yehova.
Wakati nilikuwa Australia, hali yangu ya kiroho ilishuka sana. Nilianza kukosa mikutano. Nilifanya urafiki pamoja na vijana wenye, sawa miye, walikuwa wanakusanyika usiku na kisha walienda kunywa na kucheza mu boîte de nuit. Wakati nakumbuka ile kipindi ya maisha yangu, nafikia kutambua kama nilikuwa mugulu moya ndani ya kweli na ingine inje. Lakini sikujisikia tu muzuri ikuwe ndani ao inje ya kweli.
NAMNA HALI FULANI YENYE SIKUTAZAMIA ILIBADILISHA MAISHA YANGU
Kisha miaka mbili nilizungumuza na dada mumoja mwenye alinisaidia bila yeye kujua. Ile mazungumuzo ilinisaidia niwaze sana juu ya maisha yangu. Tulikuwa dada tano wenye kuishi mu nyumba moja, na siye wote tulikuwa hatujaolewa. Na siku moja tulikaribishaka mwangalizi wa muzunguko na bibi yake, Tamara. Tulifanyaka nao juma moja ku nyumba. Wakati bwana yake alikuwa mu mambo ya kutaniko, siye na Tamara tulipitisha wakati pamoja na tulicheka sana. Nilipenda sana vile. Alikuwa dada mwenye kuhangaikia sana watu na ilikuwa mwepesi kuongea naye. Nilishangaa sana kuona mutu wa kiroho kama yeye iko anachekesha-chekesha watu.
Tamara alikuwa dada muchangamufu sana. Alipenda sana kweli na mahubiri na wakati unamuona unapenda tu kuwa sawa yeye. Alikuwa na furaha juu alimutumikia Yehova kwa uwezo wake wote, lakini miye sikukuwa na furaha juu sikumupatia kabisa Yehova kile anastahili. Namna yake ya kuwa na furaha yenye alikuwa nayo, ilinisaidia sana mu maisha yangu. Mufano wake ulinisaidia nifikirie hii jambo ya maana sana: Yehova anapenda siye wote tumutumikie “kwa furaha” na “kwa vigelegele vya shangwe.”—Zb. 100:2.
NAMNA NILIANZA TENA KUPENDA MAHUBIRI
Nilipenda kuwa na furaha kama ya Tamara, lakini iliniomba nifanye mabadiliko fulani makubwa juu na miye nikuwe na ile furaha. Iliomba wakati, lakini sikubadilika mara moja, nilienda polepole. Nilianza kujitayarisha mbele ya kuenda mu mahubiri, na wakati fulani nilikuwa nafanya kazi ya upainia musaidizi. Ile ilinisaidia nisikuwe naogopa sana na nijitumainie. Juu nilitumia sana Biblia mu mahubiri, ile ilinifanya nipende mahubiri zaidi. Na bila kukawia, nilianza kuwa painia musaidizi kila mwezi.
Nilianza kuchagua marafiki wa kila miaka wenye walikuwa wanamutumikia Yehova kwa uwezo wao wote. Mifano yao ya muzuri ilinisaidia nifikirie mambo yenye ilikuwa ya maana zaidi mu maisha yangu, na nianze kusoma Biblia kila siku. Nilianza kupenda mahubiri hata zaidi na ku mwisho nikafikia kuwa painia wa kawaida. Kisha miaka mingi, nikafikia sasa kutulia, nikapata furaha na nikaanza kujisikia kuwa mushiriki mu kutaniko.
NILIPATA PAINIA MWENYE ALINITEGEMEZA SANA
Kisha mwaka moja, nilikutana na Alex, mwanaume mupole na munyoofu, mwenye anapenda Yehova na kazi ya kuhubiri. Alikuwa mutumishi wa huduma na alikuwa alishafanya miaka sita mu kazi ya upainia. Wakati fulani, Alex alihubiri pia mu Malawi, juu kulikuwa lazima kubwa ya wahubiri. Kule alipitisha wakati pamoja na wamisionere, wenye walimuwekea mufano muzuri na wenye walimutia moyo aendelee kutia faida za Ufalme pa nafasi ya kwanza.
Mu mwaka wa 2003, miye na Alex tulioana, na tangu ile wakati tuliendelea na utumishi wa wakati wote pamoja. Tulijifunza mambo mingi ya muzuri na Yehova alitubariki mu njia mingi mbalimbali.
YEHOVA ALITUBARIKI HATA ZAIDI
Tuko mu mahubiri mu muji wa Gleno, Timor Mashariki
Mu mwaka wa 2009, tulialikwa kuwa wamisionere mu Timor Mashariki, inchi ya kidogo, katika visiwa vya Indonesia. Tulishangazwa sana, tulifurahi, na tuliogopa. Kisha miezi tano, tulifika Dili, muji mukubwa wa Timor Mashariki.
Maisha ku nyumba yetu ya mupya ilikuwa tofauti sana na maisha yenye tulikuwa nayo mbele. Tulipaswa kujikaza kuzoea desturi ya mupya, luga, chakula na hata hali ya maisha ya mupya. Mara mingi mu mahubiri tulikuwa tunaona watu wenye walikuwa maskini sana, wenye walikuwa na elimu kidogo ao hawakusoma, na wengine wenye walitendewa mubaya. Na tuliona watu wengi wenye walikuwa wanateseka kimwili na kiakili juu ya vita na mauaji.a
Mahubiri ilishangaza sana! Kwa mufano, siku moja nilikutana na Mariab, binti mumoja wa miaka 13 na alikuwa na huzuni. Kulikuwa kumepita miaka kidogo tu tangu mama yake akufe, na hakukuwa anaonana na baba yake kila mara. Sawa vile watoto wengi wa miaka yake, Maria hakujua afanye nini mu maisha yake. Nakumbuka siku moja alilia wakati alikuwa ananifasiria namna alikuwa anajisikia. Lakini, sikuelewa mambo yenye alikuwa anasema juu nilikuwa siyajua muzuri kusema luga yao. Nilisali kwa Yehova, nilimuomba anisaidie nimutie moyo, na kisha nikaanza kumusomea maandiko fulani yenye ingemufariji. Kisha miaka fulani yenye ilifuata, niliona namna kweli ilibadilisha maisha ya Maria, ni kusema, namna yake ya kuwa, namna yake ya kuvala na kujipamba na mambo ingine. Alifikia kubatizwa na sasa iko anaongoza mafunzo yake ya Biblia. Leo, Maria iko mu familia kubwa ya watu wa Yehova na anajisikia kuwa anapendwa.
Yehova iko anabariki kazi ya kuhubiri katika Timor Mashariki. Hata kama ni mu miaka 10 hivi yenye imepita njo wahubiri wengi walibatizwa, wengi wako mapainia, watumishi wa huduma, na hata wazee. Na wengine wanatumika ku biro ya kutafsiri na wanasaidia kutafsiri vichapo vyenye vinategemea Biblia mu luga za eneo lao. Nafurahi sana wakati nawaona wanaimba ku mikutano, wako na furaha na wakati naona wanafanya maendeleo ya kiroho.
Miye na Alex, tunaenda kupatia watu mialiko ya Ukumbusho mu eneo lenye halijapewa muhubiri yeyote
SIKUTAZAMIA KUWA NA MAISHA YA FURAHA KAMA HII
Maisha yetu katika Timor Mashariki ilikuwa tofauti sana na maisha ya Australia, lakini kusema kweli, sikutazamia kuwa na maisha ya furaha kama hii. Wakati fulani, tulisafiri mu bus ya kidogo yenye kujaa watu, na ndani ya ile bus mulikuwa samaki za baridi na mboga mingi za majani zenye watu waliuza ku soko. Masiku fulani, tulikuwa tunaenda kuongoza funzo la Biblia mu nyumba ya kidogo na yenye kuwa na kifukutu, chini kulikuwa buchafu, na kuku zilikuwa zinapita-pita huku na huku. Hata kama tulipata ile matatizo yote, mara mingi niliwaza hivi, ‘Hii ni maisha ya kushangaza sana!’
Wakati tuko tunaenda mu eneo
Wakati nakumbuka maisha yangu ya zamani, nashukuru sana wazazi wangu, juu walifanya yote yenye waliweza ili kunifundisha njia za Yehova na kunitegemeza, hata wakati urafiki wangu pamoja Naye haukukuwa tena muzuri. Nilijionea ukweli wa maneno ya Mezali 22:6. Leo, Mama na Baba wanafurahi sana kuona vile miye na Alex tunamutumikia Yehova. Tangu mwaka wa 2016 tuko tunatumikia mu kazi ya muzunguko mu eneo la tawi ya Autralasia.
Niko naonyesha watoto fulani wa Timor Mashariki video ya Caleb na Sophia
Ni nguvu kuamini kama wakati fulani sikukuwa nafurahia kazi ya mahubiri. Sasa napenda mahubiri! Nilifikia kutambua kama ijapokuwa mambo yenye inaweza kutufikia mu maisha, kumutumikia Mungu kwa moyo wote njo kunaleta furaha ya kweli. Kusema kweli, miaka 18 yenye imepita yenye tumemutumikia Yehova miye na Alex, ilikuwa miaka ya furaha zaidi mu maisha yangu. Naelewa sasa ukweli wa mambo yenye muandikaji wa zaburi Daudi alimuambia Yehova: “Wale wote wenye kukukimbilia watashangilia; watapiga vigelegele vya shangwe sikuzote. . . . Na wale wenye kupenda jina lako watashangilia katika wewe.” —Zb. 5:11.
Inaletaka furaha sana kujifunza Biblia na watu wanyenyekevu!
a Kuanzia mwaka wa 1975, kulikuwa vita katika Timor Mashariki juu watu walikuwa wanapigania uhuru. Ile vita ilifanya zaidi ya miaka 20.
b Jina imebadilishwa.