Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • wp23 na. 1 uku. 6-7
  • 1 | Sala—“Mumutupie Mahangaiko Yenu Yote”

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • 1 | Sala—“Mumutupie Mahangaiko Yenu Yote”
  • Munara wa Mulinzi Unatangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti ya Watu Wote)—2023
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Ile Iko na Maana Gani?
  • Namna Gani ile Inaweza Kusaidia?
  • Umutupie Yehova Mahangaiko Yako Yote
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2016
  • Biblia Inasema Nini?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2017
  • Mahangaiko
    Amuka!—2016
  • Unaweza Kufanya Nini Kama Uko na Mahangaiko?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2022
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unatangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti ya Watu Wote)—2023
wp23 na. 1 uku. 6-7
Kijana mwanaume mwenye kuwa na mahangaiko anajikamata kukifua wakati iko nasali.

1 | Sala “Mumutupie Mahangaiko Yenu Yote”

BIBLIA INASEMA HIVI: “Mumutupie [Mungu] mahangaiko yenu yote, kwa sababu yeye anawahangaikia ninyi.” —1 PETRO 5:7.

Ile Iko na Maana Gani?

Yehova anatuomba tuzungumuze naye juu ya mizigo yoyote yenye iko buzito mu akili ao mu moyo wetu. (Zaburi 55:22) Tusikose kusali juu tunawaza kama magumu yetu ni ya mukubwa sana ao ni ya kidogo sana. Kama tu inatuhangaisha siye, inamuhangaisha pia Yehova. Kusali kwa Yehova ni jambo ya maana sana yenye tunapaswa kufanya kama tunapenda tukuwe na amani ya akili. —Wafilipi 4:6, 7.

Namna Gani ile Inaweza Kusaidia?

Wakati tuko napiganisha magonjwa ya akili, tunaweza kujisikia kuwa peke yetu kabisa. Wakati fulani watu wengine wanaweza kukosa kuelewa kabisa mambo yenye tuko napitia. (Mezali 14:10) Lakini wakati tunasali kwa Mungu na kumuambia waziwazi namna tuko najisikia, atatusikiliza, atajitia pa nafasi yetu, na atatuelewa. Yehova iko anatuona, anajua maumivu yetu, na mambo yenye iko natuhangaisha na anapenda tusali kwake juu ya jambo yoyote yenye iko natuhangaisha.—2 Mambo ya Nyakati 6:29, 30.

Kuzungumuza na Yehova kupitia sala kunatusaidia tukuwe hakika zaidi kama anatuhangaikiaka. Ile inafanya tujisikie sawa mwandikaji moya wa zaburi mwenye alisali hivi: “Umeona mateso yangu; unajua taabu yangu nyingi.” (Zaburi 31:7) Kujua tu kama Yehova anaonaka mambo yenye iko natufikia inaweza kutusaidia tuvumilie magumu. Lakini, Yehova haishiake tu ku kuona mambo yenye iko natuhangaisha. Kuliko mutu mwingine yeyote, anaelewa mambo yenye iko natufikia na anatusaidia tupate mu Biblia mawazo yenye kutuliza na yenye kutia moyo. 

Namna Biblia Iko Nasaidia Julian

Namna Wasiwasi Inanihangaishaka

Julian.

“Niko na ugonjwa wa akili wenye unafanyaka nikuwe na wasiwasi na nikuwe na mawazo yenye kuhangaisha, yenye kunichochea nifanye jambo fulani juu nijisikie kuwa ninatulia. Wasiwasi inanihangaishaka bila kutazamia. Wakati fulani nakuwaka najisikia muzuri, kisha mara moya tu ninajisikia mubaya sana bila hata sababu. Nakuwaka na wasiwasi zaidi sana wakati niko pamoya na watu wengine. Saa yote nakuwaka najiuliza tu kama wako nawaza nini juu yangu.

“Watu wenye wanajuaka magumu yangu wananisaidiaka sana. Kusema kweli wakati fulani mambo yenye wanasemaka haikuwake njo mambo yenye ningependa kusikia. Lakini nafurahiaka sana kuona namna wanajikazaka kunisaidia.

“Wakati fulani ugonjwa wangu unafanyaka ikuwe nguvu kusali. Inaombaka nijikaze sana juu nikuwe na akili yenye kutulia na nisali kwa Yehova. Mawazo mingi inanipitaka mu kichwa mupaka inafanya ikuwe nguvu kwangu kukuwa na akili yenye kutulia. Wakati nashindwa kuzuia mawazo yangu, inakuwaka nguvu kumuambia Yehova mambo yenye niko nawaza na namna niko najisikia.”

Namna Biblia Inanisaidiaka

“Nimejifunza mu Biblia kama haiko lazima sala yetu ikuwe murefu ao ikuwe na maneno ya mingi yenye kupangwa muzuri juu Mungu aisikie. Wakati fulani kama nashindwa kumuambia Yehova vile niko najisikia, nakuwaka nasali tu: ‘Yehova, tafazali unisaidie.’ Hata mu ile hali, najioneaka kama Yehova anakuwaka ananielewa na ananipatiaka mambo yenye niko nayo lazima ile wakati. Na zaidi ya kusali, nimetafuta musaada wa munganga. Niko mwenye furaha juu ile mambo mbili imenisaidia nijisikie muzuri zaidi. Kusema kweli ni jambo ya maana sana kutafuta musaada wa Baba yangu wa mbinguni na kujionea namna ananitegemeza kwa upendo.”

Musaada kwa Vijana

Video “Ukuwe Rafiki ya Yehova—Sali Saa Yote.”

Ku site jw.org, ona mambo yenye itakusaidia ukuwe hakika kama Yehova anasikilizaka na kujibia sala zako.

Angalia video Ukuwe Rafiki ya Yehova —Sali Saa Yote.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine