-
Kutoka 7:5Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
5 Na Wamisri watajua kwa hakika kwamba mimi ni Yehova+ nitakapounyoosha mkono wangu dhidi ya Misri na kuwatoa Waisraeli miongoni mwao.”
-
-
Kutoka 8:9, 10Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
9 Kisha Musa akamwambia Farao: “Kwa heshima yako niambie wakati unaotaka nimwombe Mungu awaondoe vyura kutoka kwako, kutoka kwa watumishi wako, kutoka kwa watu wako, na kutoka katika nyumba zenu. Watabaki katika Mto Nile tu.” 10 Farao akamwambia: “Kesho.” Basi Musa akasema: “Itakuwa kama unavyosema, ili ujue kwamba hakuna yeyote aliye kama Yehova Mungu wetu.+
-
-
Kutoka 9:29Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
29 Kwa hiyo Musa akamwambia: “Mara tu nitakapoondoka jijini, nitainyoosha mikono yangu mbele za Yehova. Ngurumo itakoma na mvua ya mawe haitaendelea kunyesha, ili ujue kwamba dunia ni ya Yehova.+
-