Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutoka 29:1, 2
    Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
    • 29 “Hivi ndivyo utakavyowatakasa ili wanitumikie wakiwa makuhani: Chukua ng’ombe dume mchanga, kondoo dume wawili wasio na kasoro,+ 2 mikate isiyo na chachu, mikate ya mviringo isiyo na chachu na iliyokandwa kwa mafuta, na mikate myembamba isiyo na chachu na ambayo imepakwa mafuta.+ Utaioka kwa unga laini wa ngano

  • Kutoka 29:40, 41
    Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
    • 40 Sehemu ya kumi ya kipimo cha efa moja* ya unga laini uliochanganywa na robo ya hini* ya mafuta ya zeituni zilizopondwa, na toleo la kinywaji la robo ya hini ya divai, vitatolewa pamoja na mwanakondoo dume wa kwanza. 41 Utamtoa mwanakondoo dume wa pili jioni kabla ya giza kuingia,* pamoja na matoleo ya nafaka na kinywaji kama yale ya asubuhi. Utamtoa akiwa harufu inayopendeza,* dhabihu kwa Yehova inayochomwa kwa moto.

  • Mambo ya Walawi 2:1
    Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
    • 2 “‘Sasa ikiwa mtu atamtolea Yehova toleo la nafaka,+ ni lazima toleo lake liwe la unga laini, naye anapaswa kumimina mafuta juu yake na kuweka ubani juu yake.+

  • Mambo ya Walawi 9:17
    Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
    • 17 Kisha akatoa toleo la nafaka;+ akachukua mkono mmoja wa toleo hilo na kuliteketeza ili lifuke moshi kwenye madhabahu pamoja na dhabihu ya kuteketezwa ya asubuhi.+

  • Hesabu 28:4, 5
    Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
    • 4 Mtamtoa mwanakondoo dume mmoja asubuhi, na mwanakondoo dume wa pili mtamtoa jioni kabla ya giza kuingia,*+ 5 pamoja na toleo la nafaka la sehemu ya kumi ya kipimo cha efa moja* ya unga laini uliochanganywa na robo ya hini* ya mafuta ya zeituni zilizopondwa.+

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki