-
Hesabu 12:14Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
14 Yehova akamjibu Musa: “Ikiwa baba yake angemtemea mate usoni moja kwa moja, je, hangeaibika kwa siku saba? Acha atengwe nje ya kambi kwa siku saba,+ kisha anaweza kurudishwa kambini.”
-
-
2 Wafalme 7:3Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
3 Kulikuwa na watu wanne wenye ukoma kwenye lango la jiji,+ nao wakaambiana: “Kwa nini tuketi hapa mpaka tufe?
-
-
2 Mambo ya Nyakati 26:20, 21Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
20 Azaria mkuu wa makuhani na makuhani wote walipogeuka na kumtazama, waliona kwamba alikuwa amepigwa na ukoma kwenye paji la uso! Kwa hiyo wakamtoa humo haraka, naye mwenyewe akatoka nje haraka, kwa sababu Yehova alikuwa amemletea pigo.
21 Mfalme Uzia aliendelea kuwa na ukoma mpaka siku aliyokufa, naye aliendelea kukaa katika nyumba iliyotengwa akiwa mtu mwenye ukoma,+ kwa sababu alizuiwa kuingia katika nyumba ya Yehova. Yothamu mwanawe ndiye aliyesimamia nyumba ya* mfalme, akiwahukumu watu nchini.+
-