-
Kutoka 4:14-16Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
14 Ndipo hasira ya Yehova ikawaka dhidi ya Musa, akasema: “Namna gani ndugu yako Haruni,+ Mlawi? Ninajua kwamba anaweza kuzungumza vizuri sana. Na sasa yuko njiani anakuja hapa kukutana nawe. Atakapokuona, moyo wake utashangilia.+ 15 Basi unapaswa kuzungumza naye na kuweka maneno hayo kinywani mwake,+ nami nitakuwa pamoja nawe na yeye pia mnapozungumza,+ nami nitawafundisha jambo la kufanya. 16 Atazungumza na watu kwa niaba yako, naye atakuwa msemaji wako, nawe utakuwa kama Mungu kwake.*+
-
-
Kutoka 4:30Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
30 Haruni akawaambia maneno yote ambayo Yehova alimwambia Musa, naye akafanya zile ishara+ machoni pa watu.
-
-
Kutoka 15:20Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
20 Kisha nabii Miriamu, dada ya Haruni, akachukua tari, na wanawake wote wakamfuata wakiwa na matari yao wakicheza dansi.
-