-
Kumbukumbu la Torati 28:15Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
15 “Lakini msipoisikiliza sauti ya Yehova Mungu wenu kwa kuwa waangalifu kutenda amri zake zote na sheria zake ninazowaamuru leo, laana hizi zote zitawajia na kuwatangulia:+
-
-
Kumbukumbu la Torati 28:23Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
23 Anga lililo juu ya vichwa vyenu litakuwa shaba, na dunia iliyo chini yenu itakuwa chuma.+
-
-
1 Wafalme 8:35, 36Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
35 “Mbingu zikifungwa kusiwe na mvua+ kwa sababu wamezidi kukutendea dhambi,+ nao wasali kuelekea mahali hapa na kulitukuza jina lako na kuacha dhambi yao kwa sababu umewanyenyekeza,*+ 36 basi usikie kutoka mbinguni na kuwasamehe watumishi wako dhambi yao, dhambi ya watu wako Waisraeli, kwa sababu utawafundisha+ njia nzuri wanayopaswa kufuata; na ulete mvua katika nchi yako+ ambayo uliwapa watu wako kuwa urithi.
-
-
2 Mambo ya Nyakati 7:13, 14Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
13 Nikifunga mbingu ili mvua isinyeshe, nami nikiamuru panzi waile nchi, nami nikileta ugonjwa hatari miongoni mwa watu wangu, 14 na watu wangu ambao wameitwa kwa jina langu+ wakijinyenyekeza+ na kusali na kuutafuta uso wangu na kuacha njia zao ovu,+ ndipo nitakaposikia kutoka mbinguni na kuwasamehe dhambi yao na kuiponya nchi yao.+
-