-
Waamuzi 9:16-18Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
16 “Je, mmetenda kwa unyoofu na heshima kwa kumweka Abimeleki kuwa mfalme,+ na je, mmemtendea wema Yerubaali na nyumba yake, je, mmemtendea anavyostahili? 17 Baba yangu alipowapigania,+ alihatarisha uhai wake* ili kuwaokoa kutoka mikononi mwa Wamidiani.+ 18 Lakini leo mmeasi nyumba ya baba yangu na kuwaua wanawe 70 juu ya jiwe moja.+ Kisha mkamweka Abimeleki, mwana wa kijakazi wake,+ awe mfalme juu ya viongozi wa Shekemu kwa sababu tu yeye ni ndugu yenu.
-