-
Kumbukumbu la Torati 32:39Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
Mimi huua, nami hufanya kuwa hai.+
-
-
2 Wafalme 4:32Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
32 Elisha alipoingia katika nyumba hiyo, mvulana huyo alikuwa amelala kwenye kitanda chake akiwa mfu.+
-
-
2 Wafalme 4:34Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
34 Kisha akapanda kitandani na kumlalia mtoto huyo, kinywa chake kikiwa juu ya kinywa cha mvulana huyo, macho yake juu ya macho yake, na viganja vyake juu ya viganja vyake, akaendelea kumlalia, na mwili wa mtoto huyo ukaanza kupata joto.+
-
-
2 Wafalme 13:21Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
21 Wanaume fulani walipokuwa wakimzika mtu, waliona kundi la wavamizi, kwa hiyo wakamtupa mara moja mtu huyo ndani ya kaburi la Elisha na kukimbia. Mtu huyo alipogusa mifupa ya Elisha, akafufuka+ na kusimama.
-
-
Matendo 20:9, 10Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
9 Kijana aitwaye Eutiko alikuwa ameketi dirishani, naye akalala usingizi mzito Paulo alipokuwa akiongea, basi akalemewa na usingizi, akaanguka chini kutoka ghorofa ya tatu, akaokotwa akiwa amekufa. 10 Lakini Paulo akashuka kutoka ghorofani, akajitupa juu yake akamkumbatia+ na kusema: “Acheni kupiga kelele, kwa maana yuko hai.”*+
-
-
Waroma 14:9Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
9 Kwa maana kwa kusudi hili Kristo alikufa na akawa hai tena, ili awe Bwana juu ya waliokufa na walio hai pia.+
-
-
Waebrania 11:19Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
19 Lakini alifikia uamuzi kwamba Mungu angeweza kumfufua hata kutoka kwa wafu, naye alimpokea kutoka huko kwa njia ya mfano.+
-