Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kumbukumbu la Torati 32:39
    Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
    • 39 Sasa tazameni kwamba mimi—mimi ndiye,+

      Na hakuna miungu mingine ila mimi.+

      Mimi huua, nami hufanya kuwa hai.+

      Ninajeruhi,+ nami nitaponya,+

      Na hakuna anayeweza kumwokoa yeyote kutoka mikononi mwangu.+

  • 1 Samweli 2:6
    Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
    •  6 Yehova huua, naye huhifadhi uhai;*

      Hushusha Kaburini,* naye hufufua.+

  • 2 Wafalme 4:32
    Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
    • 32 Elisha alipoingia katika nyumba hiyo, mvulana huyo alikuwa amelala kwenye kitanda chake akiwa mfu.+

  • 2 Wafalme 4:34
    Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
    • 34 Kisha akapanda kitandani na kumlalia mtoto huyo, kinywa chake kikiwa juu ya kinywa cha mvulana huyo, macho yake juu ya macho yake, na viganja vyake juu ya viganja vyake, akaendelea kumlalia, na mwili wa mtoto huyo ukaanza kupata joto.+

  • 2 Wafalme 13:21
    Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
    • 21 Wanaume fulani walipokuwa wakimzika mtu, waliona kundi la wavamizi, kwa hiyo wakamtupa mara moja mtu huyo ndani ya kaburi la Elisha na kukimbia. Mtu huyo alipogusa mifupa ya Elisha, akafufuka+ na kusimama.

  • Luka 7:15
    Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • Luka 8:54, 55
    Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
    • 54 Lakini akamshika mkono na kumwita: “Mtoto, inuka!”+ 55 Roho+ yake ikarudi* naye akasimama mara moja,+ kisha Yesu akaagiza apewe chakula.

  • Yohana 5:28, 29
    Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • Yohana 11:44
    Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • Matendo 9:40, 41
    Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
    • 40 Petro akaagiza kila mtu aende nje,+ akapiga magoti na kusali. Kisha akaugeukia ule mwili, akasema: “Tabitha, inuka!” Akafungua macho yake, na alipomwona Petro, akaketi.+ 41 Petro akamshika mkono na kumwinua, akawaita watakatifu na wajane, akamkabidhi kwao akiwa hai.+

  • Matendo 20:9, 10
    Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
    • 9 Kijana aitwaye Eutiko alikuwa ameketi dirishani, naye akalala usingizi mzito Paulo alipokuwa akiongea, basi akalemewa na usingizi, akaanguka chini kutoka ghorofa ya tatu, akaokotwa akiwa amekufa. 10 Lakini Paulo akashuka kutoka ghorofani, akajitupa juu yake akamkumbatia+ na kusema: “Acheni kupiga kelele, kwa maana yuko hai.”*+

  • Waroma 14:9
    Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
    • 9 Kwa maana kwa kusudi hili Kristo alikufa na akawa hai tena, ili awe Bwana juu ya waliokufa na walio hai pia.+

  • Waebrania 11:17
    Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
    • 17 Kwa imani, Abrahamu alipojaribiwa,+ ni kana kwamba alimtoa Isaka—mtu huyo aliyekuwa amezipokea ahadi kwa furaha alijaribu kumtoa mwana wake mzaliwa-pekee+—

  • Waebrania 11:19
    Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
    • 19 Lakini alifikia uamuzi kwamba Mungu angeweza kumfufua hata kutoka kwa wafu, naye alimpokea kutoka huko kwa njia ya mfano.+

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki