-
Hesabu 11:11Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
11 Kisha Musa akamwambia Yehova: “Kwa nini unanitesa mimi mtumishi wako? Kwa nini hupendezwi nami, hivi kwamba umenitwika mzigo wa watu wote hawa?+
-
-
Hesabu 11:15Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
15 Ikiwa utaendelea kunitendea hivi, tafadhali niue sasa hivi.+ Ikiwa nimepata kibali machoni pako, usiache niendelee kutaabika.”
-
-
1 Wafalme 19:3, 4Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
3 Basi Eliya akaogopa, akaondoka na kukimbia ili kuokoa uhai wake.*+ Akafika Beer-sheba,+ jiji la Yuda,+ akamwacha mtumishi wake huko. 4 Akaingia nyikani safari ya siku moja, akafika na kuketi chini ya mti wa mretemu, naye akaomba afe. Akasema: “Imetosha! Sasa, Ee Yehova, niue,*+ kwa sababu mimi si bora kuliko mababu zangu.”
-
-
Yona 4:3Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
3 Sasa, Ee Yehova, nakusihi uniue, kwa maana afadhali nife badala ya kuishi.”+
-