-
Kutoka 16:14Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
14 Utando huo wa umande ulipotoweka, kitu laini, kinachovunjikavunjika,+ kitu laini kama theluji, kilienea kwenye ardhi nyikani.
-
-
Kutoka 16:31, 32Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
31 Watu wa nyumba ya Israeli waliuita mkate huo “mana.”* Ulikuwa mweupe kama mbegu za mgiligilani, na ladha yake ilikuwa kama ya keki bapa zenye asali.+ 32 Kisha Musa akasema: “Yehova ameamuru hivi: ‘Jazeni mkate huo katika kipimo cha omeri ili uwe kitu kitakachohifadhiwa katika vizazi vyenu vyote,+ ili watoto wenu waone mkate niliowapa mle nyikani nilipokuwa nikiwatoa katika nchi ya Misri.’”
-
-
1 Wakorintho 10:2, 3Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
2 na wote walibatizwa katika Musa kupitia wingu na bahari, 3 na wote walikula chakula kilekile cha kiroho+
-