-
Yeremia 7:23, 24Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
23 Lakini niliwaamuru hivi: “Tiini sauti yangu, nami nitakuwa Mungu wenu, nanyi mtakuwa watu wangu.+ Ni lazima mtembee katika njia yote ninayowaamuru, ili mambo yawaendee vema.”’+ 24 Lakini hawakusikiliza wala kutega sikio lao;+ badala yake walitembea katika mipango yao* wenyewe, wakifuata kwa ukaidi moyo wao mwovu,+ nao wakarudi nyuma, badala ya kwenda mbele,
-
-
Yeremia 11:7, 8Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
7 Kwa maana niliwaonya vikali mababu zenu siku niliyowatoa nchini Misri na mpaka leo hii, niliwaonya tena na tena:* “Tiini sauti yangu.”+ 8 Lakini hawakusikiliza wala kutega sikio lao; badala yake, kila mmoja wao aliendelea kuufuata kwa ukaidi moyo wake mwovu.+ Basi nikawaadhibu kulingana na maneno yote ya agano hili niliyowaamuru wafuate, lakini walikataa kuyatekeleza.’”
-
-
Mika 6:16Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
16 Kwa maana unashika sheria za Omri na matendo yote ya nyumba ya Ahabu,+
Nawe unafuata ushauri wao.
-