24 Basi watu wakaanza kumnung’unikia Musa,+ wakisema: “Tutakunywa nini?” 25 Musa akamlilia Yehova,+ naye Yehova akamwelekeza kwenye mti fulani. Alipoutupa ndani ya maji hayo, yakawa matamu.
Huko Mungu akawawekea sharti na msingi wa hukumu, na huko Mungu akawajaribu.+