-
Kumbukumbu la Torati 12:31Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
31 Msimfanyie hivyo Yehova Mungu wenu, kwa sababu mataifa hayo yanaifanyia miungu yao kila jambo linalochukiza ambalo Yehova anachukia, hata kuwateketeza motoni wana na mabinti wao kwa ajili ya miungu yao.+
-
-
2 Wafalme 16:1Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
16 Katika mwaka wa 17 wa utawala wa Peka mwana wa Remalia, Ahazi+ mwana wa Mfalme Yothamu wa Yuda akawa mfalme.
-
-
2 Wafalme 17:17, 18Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
17 Pia waliwateketeza* motoni wana wao na mabinti wao,+ wakafanya uaguzi,*+ wakatafuta ishara za ubashiri, na wakaendelea kujitoa* wenyewe kutenda maovu machoni pa Yehova, na kumkasirisha.
18 Kwa hiyo Yehova akawakasirikia sana Waisraeli hivi kwamba akawaondoa mbele zake.+ Hakumwacha yeyote abaki isipokuwa watu wa kabila la Yuda peke yao.
-
-
Yeremia 7:30, 31Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
30 ‘Kwa maana watu wa Yuda wametenda maovu machoni pangu,’ asema Yehova. ‘Wameziweka sanamu zao zinazochukiza katika nyumba ambayo imeitwa kwa jina langu, ili kuitia unajisi.+ 31 Wamejenga mahali pa juu pa Tofethi, palipo katika Bonde la Mwana wa Hinomu,*+ ili kuwateketeza motoni wana wao na mabinti wao,+ jambo ambalo sikuamuru na ambalo hata halijawahi kamwe kuingia moyoni mwangu.’*+
-