-
Kumbukumbu la Torati 15:7, 8Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
7 “Ikiwa mmoja wa ndugu zenu atakuwa maskini miongoni mwenu katika mojawapo ya majiji yaliyo katika nchi ambayo Yehova Mungu wenu anawapa, msiifanye mioyo yenu iwe migumu au kumfumbia mkono ndugu yenu maskini.+ 8 Kwa maana mnapaswa kumfumbulia mkono wenu kwa ukarimu+ na kufanya yote mwezayo kumkopesha* chochote anachohitaji au alichopungukiwa.
-
-
Zaburi 41:1Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
41 Mwenye furaha ni mtu yeyote anayemjali mtu wa hali ya chini;+
Yehova atamwokoa siku ya msiba.
-
-
Luka 6:34, 35Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
34 Pia, mkiwakopesha* wale tu ambao mnatumaini watawalipa, mnapata faida gani?+ Hata watenda dhambi huwakopesha watenda dhambi ili warudishiwe kiasi kilekile. 35 Badala yake, endeleeni kuwapenda adui zenu, kutenda mema, na kukopesha bila kutumaini kurudishiwa;+ nanyi mtapata thawabu kubwa, na mtakuwa wana wa Aliye Juu Zaidi, kwa sababu yeye huwaonyesha fadhili hata watu wasio na shukrani na waovu.+
-