-
Kutoka 17:6Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
6 Tazama! Nitakuwa nimesimama mbele yako kwenye mwamba huko Horebu. Unapaswa kuupiga mwamba huo, na maji yatatoka ndani yake, kisha watu watayanywa.”+ Musa akafanya hivyo mbele ya wazee wa Israeli.
-
-
Hesabu 20:11Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
11 Ndipo Musa akainua mkono wake na kuupiga mwamba huo mara mbili kwa fimbo yake, na maji mengi yakaanza kububujika, watu wakaanza kunywa pamoja na mifugo yao.+
-
-
Kumbukumbu la Torati 8:14, 15Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
14 msiache mioyo yenu iwe na kiburi+ na kuwafanya mumsahau Yehova Mungu wenu, aliyewatoa nchini Misri, kutoka katika nyumba ya utumwa,+ 15 aliyewafanya mtembee katika nyika kubwa na yenye kutisha,+ iliyo na nyoka wenye sumu na nge na ardhi iliyokauka isiyo na maji. Alifanya maji yatiririke kutoka katika mwamba mgumu+
-
-
Zaburi 107:35Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
35 Yeye hulibadili jangwa kuwa madimbwi ya maji yenye matete,
Na nchi kavu kuwa chemchemi za maji.+
-