-
Mathayo 21:7-9Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
7 Wakamleta huyo punda na mwanapunda wake, kisha wakatandika juu yao mavazi yao ya nje, naye akayakalia.+ 8 Wengi katika umati wakatandaza mavazi yao ya nje barabarani,+ na wengine wakakata matawi ya miti na kuyatandaza barabarani. 9 Isitoshe umati uliomtangulia na wale waliomfuata waliendelea kupaza sauti: “Tunaomba umwokoe, Mwana wa Daudi!+ Amebarikiwa yule anayekuja katika jina la Yehova!*+ Tunaomba umwokoe, katika vilele vilivyo juu!”+
-
-
Marko 11:7-10Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
7 Wakampelekea Yesu huyo mwanapunda,+ wakatandika mavazi yao ya nje juu yake, naye akaketi juu yake.+ 8 Pia, wengi wakatandaza mavazi yao ya nje barabarani, lakini wengine wakatandaza matawi ya miti waliyokata katika mashamba.+ 9 Watu waliokuwa mbele na wale waliofuata nyuma wakaendelea kupaza sauti: “Tunaomba umwokoe!+ Amebarikiwa yule anayekuja katika jina la Yehova!*+ 10 Umebarikiwa Ufalme unaokuja wa baba yetu Daudi!+ Tunaomba umwokoe, katika vilele vilivyo juu!”
-