Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutoka 7:20
    Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
    • 20 Mara moja Musa na Haruni wakafanya kama Yehova alivyowaamuru. Akaiinua fimbo hiyo na kuyapiga maji ya Mto Nile mbele ya Farao na watumishi wake, na maji yote yaliyokuwa katika Mto Nile yakabadilika na kuwa damu.+

  • Kutoka 8:6
    Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
    • 6 Basi Haruni akaunyoosha mkono wake juu ya maji ya Misri, na vyura wakaanza kuja na kuifunika nchi ya Misri.

  • Kutoka 8:17
    Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
    • 17 Nao wakafanya hivyo. Haruni akaunyoosha mkono wake uliokuwa na fimbo yake na kuyapiga mavumbi ya ardhi, na mbu wakawavamia wanadamu na wanyama. Mavumbi yote katika nchi yote ya Misri yakawa mbu.+

  • Kutoka 9:6
    Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
    • 6 Na kesho yake Yehova akafanya hivyo, kila aina ya mifugo ya Wamisri ikaanza kufa,+ lakini hakuna mnyama hata mmoja wa Waisraeli aliyekufa.

  • Kutoka 9:10
    Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
    • 10 Basi wakachukua masizi kutoka katika tanuru* na kusimama mbele ya Farao, naye Musa akayarusha hewani, nayo yakawa majipu yenye usaha yaliyotokea kwenye miili ya wanadamu na wanyama.

  • Kutoka 9:23
    Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
    • 23 Kwa hiyo Musa akainyoosha fimbo yake kuelekea mbinguni, na Yehova akaleta ngurumo na mvua ya mawe, na moto* ukashuka duniani, na Yehova akafanya mvua ya mawe iendelee kunyesha juu ya nchi ya Misri.

  • Kutoka 10:12
    Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
    • 12 Sasa Yehova akamwambia Musa: “Unyooshe mkono wako juu ya nchi ya Misri ili nzige waje juu ya nchi ya Misri na kula mimea yote nchini, kila kitu ambacho hakikuharibiwa na mvua ya mawe.”

  • Kutoka 10:21
    Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
    • 21 Basi Yehova akamwambia Musa: “Unyooshe mkono wako kuelekea mbinguni ili giza liifunike nchi ya Misri, giza zito sana hivi kwamba linaweza kuguswa.”

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki