-
2 Mambo ya Nyakati 36:15, 16Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
15 Yehova Mungu wa mababu zao aliendelea kuwaonya kupitia wajumbe wake, aliwaonya tena na tena, kwa sababu aliwahurumia watu wake na makao yake. 16 Lakini waliendelea kuwadhihaki wajumbe wa Mungu wa kweli,+ wakadharau maneno yake+ na kuwakejeli manabii wake,+ mpaka ghadhabu ya Yehova ilipokuja dhidi ya watu wake,+ hivi kwamba hawangeweza kuponywa.
-
-
Isaya 42:24, 25Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
24 Ni nani aliyemtia Yakobo mikononi mwa watekaji nyara
Na Israeli mikononi mwa waporaji?
Je, si Yehova, Yule ambaye tumemtendea dhambi?
25 Basi Yeye akaendelea kummwagia ghadhabu,
Hasira yake na ghadhabu ya vita.+
Iliteketeza kila kitu kumzunguka, lakini hakulikazia jambo hilo fikira.+
Iliwaka dhidi yake, lakini hakulitia jambo hilo moyoni.+
-