-
Yeremia 25:9Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
9 ninaziita familia zote za kaskazini,”+ asema Yehova, “ninamwita Mfalme Nebukadneza* wa Babiloni, mtumishi wangu,+ nami nitawaleta dhidi ya nchi hii+ na dhidi ya wakaaji wake na dhidi ya mataifa haya yote yanayozunguka.+ Nitawaangamiza na kuwafanya kuwa kitu cha kutisha na kitu cha kupigiwa mluzi na magofu ya kudumu.
-
-
Yeremia 27:6Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
6 Na sasa mimi mwenyewe nimezitia nchi hizi zote mikononi mwa mtumishi wangu Mfalme Nebukadneza+ wa Babiloni; nimempa hata wanyama wa mwituni ili wamtumikie.
-
-
Ezekieli 29:19, 20Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
19 “Kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Ninampa Mfalme Nebukadneza* wa Babiloni nchi ya Misri,+ naye atabeba utajiri wake na kuchukua nyara kwa wingi na kuipora; na vitu hivyo vitakuwa malipo ya jeshi lake.’
20 “‘Kama malipo ya kazi kubwa aliyofanya ya kushambulia Tiro, nitampa nchi ya Misri kwa sababu walitenda kwa ajili yangu,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.
-